RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

08.01.2017: WATU WAAMUA KUOKOKA NA KUBATIZWA KWA MAJI MENGI KATIKA KANISA LA MLIMA WA MOTO MIKOCHENI "B"


Katika kanisa la Mlima wa Moto Mikocheni "B" siku ya Jumapili 08.01.2017 watu waliweza kubatizwa maji mengi baada ya kuongozwa sala ya toba na kuombewa na watumishi wa Mungu katika ibada ya Kukabidhi Malengo na Mipango yetu Kwa Mungu" iliyoongozana na ugawaji wa kalamu na peni kwa wanafunzi.

Baadhi ya waliobatizwa siku hiyo walitokawa na mapepo na majini yaliyokuwa yanawatesa kwa muda mrefu sana. Hawa wameweza kutimiza ahadi yote kama alivyobatizwa Yesu na Yohana mbatizaji.

Tunakukaribisha sana katika ibada ya Jumapili hii saa 3 asubuhi hadi saa 8 mchana. Usafiri ni bure kutoka nje kidogo cha mabasi Makumbusho au mwenge kwenye mataa. Mungu akubariki sana