Bishop aliweza kuwagawia wazee wa kanisa na baadae kwa waumini na wageni wote waliofika kanisani kumtukuza Mungu wetu. Kanisa hili limekuwa likifanya zoezi hili la ugawaji wa mbegu na watu wamekuwa wakifanikiwa katika kazi zao na ofisi zao. Mungu ni mwema sana kwani amekuwa mwaminifu sana kwa waliowaaminifu kwake. Na kupitia mbegu hii iliyotolewa Jumapili tunasubiri majibu kutoka kwa Bwana, kwani imani yetu ni kwamba Bwana amesikia na amepokea maombi yaliyoombwa na watumishi wa MUNGU.
Sasa nikuombea Jumapili hii usikose katika ibada itakayoanza saa 3 asubuhi hadi saa 8 mchana. Mungu ana kitu cha kufanya kwako siku hii maalum. Usafiri ni bure kabisa kuanzia kituo cha mabasi cha Makumbusho jijini dar es salaam au Mwenge kwenye mataa, utayaona magari yetu ya Mlima wa Moto Mikocheni "B" au utasikia watu wakisema kwa mama Gertrude Rwakatare, ingia huo, na baada ya ibada utarudishwa kituo bila ya nauli