RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

12.02.2017: VOCAPELLA WAFANYA "WONDERS" KATIKA IBADA YA KUONDOLEWA AIBU - MLIMA WA MOTO MIKOCHENI "B" SIKU YA JUMAPILI

Jamani kuna watu ambao hakika Mungu anawatumia kupitia vipaji alivyowapa. Jumapili 12.02.2017 waimbaji ambao wanaimba bila kutumia vifaa vya muziki, wanaojiita VOCAPELLA waliweza kuwashangaza na kuwabariki waumini na wageni waliofika katika kanisa la Mlima wa Moto Mikocheni "B" kwa ibada ya KUONDOLEWA AIBU. Waimbaji hawa walipopaza sauti zao tu kanisa zima lilishangaa sana jinsi waimbaji hawa wanavyoweza kuchezea sauti zao huku wakitoa ujumbe wenye kuinua imani za watu. Ibada ilikuwa njema sana, na tuna kil sababu ya kutenga dakika chache kuwaombea hawa waimbaji. Mungu awabariki sana.