RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

23.04.2017: MH. BISHOP DR. GERTRUDE RWAKATARE AWATAKA WATU KUWA NA UMONA NA LUGHA MOJA NDANI YA KANISA.

Siku ya Jumapili 23.04.2017 ya KIPOKEA HABARI NJEMA katika  kanisa la Mlima wa Mlima wa Moto Mikcheni “B”, Mh. Bishop Dr. Gertrude Rwakatare alisisitiza kanisa kuwa na umoja na kuwa na lugha moja, na hivi ndivyo alivyoanza kusema;
Bwana asifiwe sana. Tusome Neno la Mungu kitabu cha Mwanzo 11:1-9, Biblia inasema, “ Nchi yote ilikuwa na lugha moja na usemi mmoja ikawa watu waliposafiri, pande za mashariki waliona nchi tambarare katika nchi ya Shinari wakakaa huko. Wakaambiana, haya na tufanye matofari tukayachome moto. Walikuwa na matofali badala yam awe, na lami badala ya chokaa. Wakasema, haya na tujijengee mji na mnara na kilele chake kifike mbinguni, tujifanyie jina, ili tusipate kutawanyika usoni pa nchi yote. Bwana akashuka ili auoni mji na mnara, waliokuwa wakiujenga wanadamu. Bwana akasema Tazama watu hawa ni taifa moja na lugha yao ni moja na haya ndiyo wanayoanza kufanya, wala sasa hawatazuiliwa neno wanalokusudia kulifanya. Haya na tushuke  huko tuwachafulie usemi wao ili wasisikilizane maneno wao kwa wao. Basi Bwana akawatawanya kutoka huko waende usoni pa nchi yote, wakaacha kuujenga ule mji. Kwa sababu hiyo jina lake likaitwa Babeli, maana hapo ndipo Bwana alipoichafua lugha ya dunia yote, na kutoka huko Bwana akawatawanya, waende usoni pa nchi yote.”

Nitasema kwa ufupi, lakini lengo la ujumbe huu ni tuombe kwa ajili ya kanisa letu. “Ninaomba kwa ajili ya umoja wa kanisa, ninaomba kwa ajili ya mshikamano wa kanisa letu.”  Nilipokuwa safari (afrika Kusini) Mungu alisema na mimi utakaporudi  nyumbani, chukua muda mwingi hata kama ni mwezi mzima kuligusa kanisa, kugusa mioyo ya kila mmoja waweze kurudi katika upendo ule wa kwanza tulioanza nao.

Ndugu zangu tulipewa amri mpya katika Yohana 13:34 Yesu kasema,  “amri mpya nawapa pendaneni”, anasema pendaneni mpaka wamataifa wajue kweli ninyi ni wanafunzi wangu. Na kweli ukiingia katika kanisa la watu wa Mungu kitu cha kwanza kitakachokugusa ni upendo wao kwa sababu hata kama hakujui atakuuliza, na mimi nilitokea katika dini ya Romani Katoliki ambako watu wanaposalimiana wanakumbatiana kama ishara ya upendo. Nilipokuwa Katoliki baadae nikaanza kuelewa kuwa ule ulikuwa ni upendo wa kweli, waliwatambua wapendwa Wakristo kwa sababu ya kupendana kwao.

Upendo ule wa kwanza urudi tena nyumbani mwa BWANA, tukitoka nje tusisalimiane tu tunaojuana, tusalimiane na wageni, wakina mama, wamama, wengine wanakuja kanisani lakini hawana upendo wa kweli. Kama wewe unakaa kule shuka nenda kamtafute mama mwingine awe rafiki yako, tusikae wenyewe kwa wenyewe tu, kanisa litaongezeka kama kila mtu atachukua rafiki nyumbani mwa Bwana. Umoja unamtisha hata Mungu, na umoja ndio ulioweza kusimamisha falme za Kiarabu, falme za Kiarabu ziliweza kusimama kwa sababu walikuwa na umoja hawakuweza kumtoa Sadam Husseni kwa sababu walikuwa na umoja, walikuwa na mshikamano, walimpenda, hawakuweza kumtoa Gadafi kwa sababu walikuwa na mshikamano, lakini mitandao ilivyokuja, na utandawazi ulivyokuja vijana wakaanza kutuma message kuwa hawa wazee yaani Sadam na Gadafi tuwatoe madarakani  na ndio ukaona falme za Uarabuni zikaanza kusambaratika.

 Umoja unafanya tusimame pamoja, na Yesu kabla ya kuondoka kitabu cha Mathayo 17 kinasema,  akasema, “Nimewaombea hawa wachache ambao wao wamemwamini Kristo, wawe na umoja kama sisi tulivyo na umoja, umoja ni nguvu ya kanisa, hapa tunaona wenzetu katika kitabu cha Mwanzo 11, walikuwa wameshikamana wakiwa na lugha moja nia moja ya kujenga mnara mmoja ili wakamuone Mungu, wakaanza kujenga, Mungu alivyochungulia akaona mnara karibu unatoboa, akasema hawa watu tusipoenda kutawanya mbinu zao, hakika wataingia hapo. Na ndio leo hii unaona kuna lugha tofauti kama vile Kinyakyusa na lugha mbalimbali ziliingia.  Anasema wakashindwa kusikilizana, kiongozi akisema,  leta tofali huyu analeta panga yaani analeta kitu tohfauti kwasababu hawasikilizani kutokana na lugha kusambaratishwa, kuanzia hapo  kujenga mnara kukaisha hapo wakaamua wakabomoa mnara wao.

Katika kila ushirika kama hakuna lugha moja, nia moja hamuwezi kufaulu, lakini mkishikamana mtafanya makubwa. Sisi ni familia ya Kristo, sisi ni watu wa Mungu ni mfano kwa wamataifa, tukishikamana tutafanya makubwa, tukishikamana watajua kuwa tumeokoka, tukishikamana Dar es Salaam itaokoka, tukishikamana kanisa hili tutalivunja tutajenga kanisa la ghorofa, bila kujari unapesa au hauna pesa, tukishikamana watu wengi wataongezeka kanisani kwa sababu wataona tumeokoka, watu wengi wanaangaliaga hawa watu wapoje, wakiona tun watu hawaelewani wahawezi kuja kanisani lakini wakiona watu tumeshikamana, tuna umoja, tunatembelea kama hivi tunatembeleana, hapo ndipo unakuta mtu anasema hii familiya nzuri acha nijiunge nayo kwahiyo ningependa kukuasa hata kwa viongozi, sisi ndio barua iliyowazi kwa wengine, lazima sisi kwa sisi tushikamane, lazima sisi wenyewe tupendane, mmeacha historia, mmeacha mtetemeko Dodoma, mmeacha simulizi Dodoma kwa ajili ya umoja wa kanisa hili viongozi mbalimbali wanakuja walikuja ili kuungana nasi katika sherehe hii ya furaha   ya kuapishwa kwangu huu ni umoja wetu wa kanisa, wanasema jamani hawa watu ni wa namna gani, wale waliovaa sale nyekundu wakapiga picha, watu wakasema mama yangu ni nini hiki sijawahi ona, wakina baba wameva suti zao nyeusi ta tai nyekundu watu wakashangaa kwa sababu ya umoja nawasihi ndugu zangu mbalimbali, karibuni Mlima wa Moto, kanisa ni safina, ndani ya safina kuliingia nyoka, ndege, samba, mbwa, kuliingia wanyama wa kila aina wawili kwa wawili, lakini midomo ilifungwa ya samba asione mbuzi, midomo ilifungwa asiweze kummeza mbwa, unajua kiasilia mbwa na chatu, kama kuna kumaku, chatu akiachama mdomo mbwa analia mwenyewe anajipelea anajua anaenda kumezwa sasa sumaku inamvuta, lakini midomo ya chatu ilifungwa kwa sababu ilikuwa kwa ajili ya umoja na hapa kanisani kwetu sisi tuwefamiliya moja lazima tuwe wamoja aliyejuu ashuke ammbebe wa chini tukisaidiana kanisa tutasonga mbele, tukibebana kanisa litaendelea tuko hapa kwa ajili ya kusaidiana, tuko hapa kwa ajili ya kuujenga mwili wa Kristo, huwezi kumuona Mungu mzimamzima lakini mimi nitakapo kusaidia ndio Mungu ananitumia kwa mfano wake tu, kwa hivyo lazima tujishuhulishe katika misingi ya kupendana, kushikamana, kuchukuliana tofauti zetu tuziache, sisi ni ndugu, sisi ni wamoja, mimi nikipata na yeye kapata ndio maana tunachukua simu zenu, mkiwa na shida msikwame tukusaidie ili tukubebe, tukukwamue, mimi ni mama yenu wa kiroho na mama lazima nijari maisha yako. Mungu anajari umoja, na Mumngu anajali tunapochukuliana na Mungu anaribariki kanisa ukisoma Matendo 2:41 Nao waliolipokea neno lake wakabatizw, na siku ile wakaongezeka watu wapata elfu tatu. Wakawa wakidumu katika fundishola mitume na katika ushirika na katika kuumega mkate na katika kusali. Kila mtu akaingiwa na hofu, ajabu nyingi na ishara zikafanywa na mitume. Na wote walioamini walikuwa mahali pamoja na kuwa na vitu vyote shirika, wakauza mali zao na vitu vyao walivyokuwa navyo na kuwagawia watu wote kama kila mtu alivyokuwa na haja. Na siku zote kwa moyo mmoja, walidumu ndani ya hekalu, wakimega mkate nyumba kwa nyumba na kushiriki chakula chao kwa furaha na kwa moyo mweupe. Wakimsifu Mungu na kuwapendeza watu wote. Bwana akalizidisha kanisa kila siku kwa wale waliokuwa wakiokolewa. Umoja ukaleta maajabu nyumbani mwa Bwana, Mungu anashuka na anaonekana.        


Mh. Bishop Dr. Gertrude Rwakatare