RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

Habari kutoka BBC Swahili:Juma la wasiwasi kuhusu Marekani na Korea Kaskazini

Hivi ni viunganisho vya nje na vitafungua katika dirisha mpya
Haki miliki ya pichaGETTY IMAGES

Ukafuatilia matukio, mijadala na ujumbe katika mitandao ya kijamii, unaweza kudhani Vita Vikuu vya Tatu vya Dunia vinakaribia.

Rais wa Marekani Donald Trump na Kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong-un wamekuwa wakijibizana vikali kuhusu mpango wa Korea Kaskazini kuendelea kustawisha silaha za nyuklia na pia kufanyia majaribio makombora, jambo ambalo taifa hilo haliruhusiwi na Umoja wa Mataifa.

Marekani ilituma kundi la meli zake za kivita karibu na Korea Kaskazini, jambo ambalo liliikera Korea Kaskazini.

Uhusiano kati ya nchi hizo mbili haujakuwa mzuri tangu kumalizika kwa Vita Vikuu vya Pili vya Dunia.

Hata hivyo wiki iliyopita uhasama ulizidi na kufikia kiwango cha juu kuliko awali.

Jumatatu - Meli za kivita za MarekaniHaki miliki ya pichaREUTERS

Rais Trump aliagiza kundi la meli za kivita za Marekani pamoja na meli moja yenye uwezo wa kubeba ndege na pia kutumiwa na ndege hizo kupaa na kutua, zielekee upande wa Korea Kaskazini.

Taifa hilo limetekeleza majaribio kadha ya silaha za nyuklia na hilo halijaifurahisha Marekani.

Rais Trump alisema Marekani imejiandaa kuchukua hatua kivyake, bila usaidizi wa China, kukabiliana na tishio la nyuklia kutoka kwa Korea Kaskazini.

Jumanne - Kim amjibu TrumpHaki miliki ya pichaAFP

Kim Jong-Un hakufurahishwa na hayo na alimjibu vikali Bw Trump.

Wizara yake ya mambo ya nje ilinukuliwa ikisema hatua hiyo ya Marekani ni ya "kipumbavu" na ikaahidi kujilinda "kwa nguvu zote za kivita."

China, ambao ni mshirika wa karibu zaidi wa Korea Kaskazini, walionya kwamba wataingilia kati na kutoa adhabu kali zaidi za kifedha kwa Korea Kaskazini iwapo taifa hilo lingefanya majaribio zaidi ya makombora.

Jumatano - China yazungumzaHaki miliki ya pichaREUTERS

Vyombo vya habari vya China vilisema rais wa taifa hilo alimpigia Rais Trump kutuliza hali.

Rais Trump mwenyewe aliandika kwenye Twitter kwamba alikuwa amewasiliana na Rais Xi Jinping.

Bw Xi alidaiwa kumwambia Trump kwamba anataka amani na utahibiti eneo hilo na kwamba anaunga mkono pia juhudi za kumaliza silaha za nyuklia katika rasi ya Korea.

Alhamisi- Gwaride la wanajeshiHaki miliki ya pichaAFP

Korea Kaskazini ilizindua mpango wake mpya wa ujenzi wa nyumba za makazi na biashara mjini Pyongyang.

Ulionekana kuwa mpango wa kawaida tu, lakini ilikuwa pia fursa ya taifa hilo kuonyesha nguvu zake.Haki miliki ya pichaREUTERS

Waandishi wa habari wa mashirika ya kigeni walialikwa kushuhudia wanajeshi wakifanya gwaride na kutembea kwenye barabara za mji huo.

Donald Trump hakufurahishwa na hilo.

Aliandika tena kwente Twitter kwamba Marekani iko tayari kukabiliana na Korea Kaskazini.

Ijumaa- Onyo la ChinaHaki miliki ya pichaAFP

China ilitahadharisha kwamba mzozo mkubwa kati ya Marekani na Korea Kaskazini "unaweza kutokea wakati wowote".

Ilizionya nchi zote mbili kukoma kurushiana vitisho, na kusema hakuwezi kuwa na mshindi katika vita.

Hayo yakijiri, Korea Kaskazini ilikuwa inakamilisha maandalizi ya gwaride kubwa na maonyesho ya kijeshi Jumamosi.

Jumamosi - Vifaru barabaraniHaki miliki ya pichaAFP

Korea Kaskazini iliadhimisha miaka 105 tangu kuzaliwa kwa mwanzilishi wa taifa hilo Kim Il-sung.

Vifaru zilitolewa barabara za Pyongyang. Serikali ya Korea Kaskazini pia ilionyesha hadharani kwa mara ya kwanza makombora yanayoweza kuruka kutoka bara moja hadi jingine, na pia makombora ya masafa marefu yanayoweza kurushwa kutoka kwenye nyambizi.Haki miliki ya pichaAFP

Maafisa wa serikali ya Korea Kaskazini waliionya Marekani dhidi ya kuchukua hatua zozote, wakisema nchi hiyo iko tayari kwa vita.

Walisema watajibu kwa "mashambulio ya nyuklia".

Hayo yakijiri, Makamu wa Rais Mike Pence alielekea Korea Kusini kujadiliana na washirika wa Marekani kuhusu njia bora zaidi za kukabiliana na Korea Kaskazini.

Jumapili - Jaribio la makomboraHaki miliki ya pichaAFP

Marekani ilidai kwamba Korea Kaskazini ilijaribu kurusha kombora, lakini likalipuka sekunde chache baada ya kupaa angani.

Inasadikika kwamba lilikuwa kombora la masafa marefu, ambalo hupaa juu anagani kwanza na ambalo huelekezwa, lakini baadaye huanguka hadi pahali ambapo panalengwa kutokana na mvuto wa dunia.

Umoja wa Mataifa umeipiga marufuku Korea Kaskazini kufanya majaribio kama hayo.

Rais Trump atachukua hatua gani?

Ni yeye mwenyewe pekee ajuaye jibu - au labda mwenyewe binafsi amekanganyikiwa!