RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

14.05.2017: VICTOR AMVISHA PETE YA UCHUMBA FATMA KANDORO KATIKA KANISA LA MLIMA WA MOTO MIKOCHENI "B" SIKU YA JUMAPILI

Muweka hazina wa vijana wa kanisa la Mlima wa Moto Mikocheni "B" Bwana Victor katika ibada ya kuwaombea mama zetu (Mother's Day) aliweza kumvisha pete ya uchumba mpenzi wake Fatma Kandoro katika kanisa la Mlima wa Moto Mikocheni "B" kwa Mh. Bishop Dr. Gertrude Rwakatare. Ukimuamini Mungu na kumtumikia naye hatakuacha kukutimizia ndoto yako. Karibuni Mlima wa Moto Mikocheni "B" kila Jumapili saa 3 asubuhi hadi saa 8 mchana na katikati ya wiki ni saa 9 mchana hadi saa 1 jioni. Upo muujiza wako kwako wewe unayetamani kuoa au kuolewa. Fatma na Victor walijiunga na kanisa hili wakiwa single na leo hii Mungu ameweza kutimiza maombi yao. Ibada za Mlima wa Moto Mikocheni "B" ni kwa dini zote, makabila yote na mataifa yote bila kujali rangi ya mtu. Mungu ni Mungu wa Wote...


































 







 xxx