RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

11.06.2017: BISHOP DR. GERTRUDE RWAKATARE AWASIMIKA WACHUNGAJI WASAIDIZI WA KANISA LA MLIMA WA MOTO MIKOCHENI "B"

Hii ni siku ambayo haitasaulika kwa wana Mlima wa Moto Mikocheni "B" pamoja na watumishi wa Mungu hawa waliosimikwa rasmi kuwa wachungaji wasaidizi wa kanisa la Mlima wa Moto Mikocheni "B"  siku ya Jumapili 11.06.2017. Mhe. Bishop Dr. Rwakatare aliweza kuwaita madhabahuni na kuwaombea kwa Mungu ili Mungu awasaidie kusimama imara kwa kazi ya Mungu. 
Hii ilifanyika katika ibada ya "NEEMA YA KUANZA UPYA"

Kama mtumishi wa Mungu tunaomba sana uzidi kuwaombea hawa wachungaji ili wasonge mbele kwa kazi ya Mungu. Pia tukukaribishe katika ibada ya Jumapili hii Mlima wa Moto Mikocheni "B", ibada itaanza saa 3 asubuhi hadi saa 8 mchana. Usafiri wa kuja kanisani ni bure kuanzia kituo cha mabasi cha Makumbusho au Mwenge kwenye mataa barabara ya Coca Cola. Mungu na akubariki sana.