RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

Cheick Tiote: Mchezaji wa zamani wa Newcastle afariki dunia


Cheick Tiote alichezea Newcastle mechi 156 mashindano yote

Kiungo wa zamani wa timu ya Newcastle United Cheick Tiote amefariki dunia akiwa an miaka 30 baada ya kuzimia wakati wa mazoezi nchini China, msemaji wa mchezaji huyo amesema.

Mchezaji huyo wa kimataifa wa Ivory Coast alikaa miaka saba Newcastle na kuwachezea mechi 138 ligini.

Alihamia klabu ya Beijing Enterprises mwezi Februari.

"Ni kwa huzuni kubwa ambapo ninathibitisha kwamba Cheick Tiote alifariki mapema leo baada ya kuzimia wakati wa mazoezi," msemaji wake alisema.

"Hatuwezi kusema zaidi kwa sasa na tunaomba kwamba familia yake iheshimiwe kipindi hiki kigumu. Tunaomba maombi yenu."

Tiote alizaliwa Ivory Coast na alikuwa kwenye kikosi kilichoshinda Kombe la Mataifa ya Afrika 2015.