RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

Kanisa Ghana laandaa ibada kusherehekea ushindi wa Chelsea


Kasisi Azigiza alimshukuru Mungu kwa ufanisi wa Chelsea


Kanisa moja katika mji mkuu wa Ghana, Accra, limeandaa ibada ya kutoa shukrani kutokana na ufanisi wa hivi majuzi wa Chelsea katika Ligi ya Premia.

Mchungaji Azigiza ambaye ni shabiki damu wa klabu hiyo aliwahamisha waumini wafike kwa ibada wakiwa wamevalia fulana za klabu hiyo.

Alisimama juu ya keki ya Chelsea kwenye jukwaa ambalo lilikuwa limejengwa kufanana na uwanja wa soka.

Alisema: "Chelsea, kwa kudura zake Mungu, walimaliza wa kwanza."

Aliambia BBC kwamba alitaka kutumia nguvu za soka kuzungumzia kuhusu Mungu.

Azigiza pia aliongoza waumini kuimba aya ya wimbo wa klabu ya Chelsea, Blue is the Colour.

Pasta huyo, ambaye wakati mmoja alikuwa DJ wa redioni, alikuwa pia anamtania mkuu wake katika kanisa hilo la Living Streams International Church, Pasta Ebenezer Markwei, ambaye ni shabiki wa Arsenal, na ambaye alikuwa amemkaribisha kwa ibada hiyoMKuu wa awali wa Pasta Azigiza, Ebenezer Markwei (kulia) ni shabiki wa Arsenal

Pasta Markwei alitoa mahubiri kuhusu "mema, mabaya na maovu ya ushindani" akidokeza kwamba mashabiki wa soka wanafaa kushiriki katika ushindani mwema.

Alisema kuna mambo mema sana katika kfuurahia ufanisi wa watu wengine.Mashabiki wa klabu mbalimbali walihimizwa kukumbatianaKanisa hilo lilitaka kuhamaisha kuhusu uzuri wa ushindani mwema

Chelsea walishindwa na Arsenal 2-1 katika fainali Kombe la FA.Hakukuwa na shaka kwamba ilikuwa ibada ya kusherehekea ushindi wa ChelseaWacheza ngoma wakicheza kwa wakati wa kuchezwa kwa wimbo wa Chelsea