RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

PAUL CLEMENT, GOODLUCK GOZBERT NA ANGEL BERNARD KUIWAKILISHA TANZANIA KATIKA SAUTI AWARDS NCHINI MAREKANI.



Moja kati ya story zinazotrend katika wiki hii ni pamoja na hii ambapo wanamuziki Paul Clement (Amenifanyia amani) pamoja na Goodluck Gozbert (Wacha waambiane) kuchaguliwa katika awards zinazofanyika nchini Marekani kila mwaka zinazofahamika kama Sauti Awards.
Goodluck Gozbert

Akiongea na Zegospel mwanamuziki Paul Clement amesema kuwa ni jambo la kumshukuru sana Mungu katika hatua hiyo kwani kazi zao pia zinazidi kupata kibali mbele za Mung na kuzidi kuvuka mipaka, Katika awards hizo hizo mwanadada Angel Bernard pamoja na Mercy Masika wako kwenye kinyang’anyiro cha the song of the year na nyimbo yao Huyu Yesu huku Goodluck akiwa katika kinyang’anyiro cha male artist of the year.
Angel Bernard na Mercy Masika