RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

18.06.2017: MH. MARY MWANJELWA (MBUNGE) AWEKA WAZI SIFA ZA RAIS DKT. JOHN MAGUFULI.

Mh. Dkt. Mary Mwanjelwa siku ya Jumapili 18,06.2017 akiwa katika kanisa la Mlima wa Moto Mikocheni “B” wakati wa ibada ya kumuombea Rais Dkt. John P.Magufuli alikuwa na haya ya kusema akiwa madhabahuni, “Bwana Yesu apewe sifa!! Nimehemewa na ufunuo wa kanisa la Mlima wa Moto Mikocheni ”B” ukiongozwa na Mama yetu Mh. Bishop Dkt. Gertrude Rwakatare kwa kutengea muda kwaajili ya kuliombea Taifa la Tanzania, serikali ya awamu ya tano na kumuombea mpendwa wetu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli. Ni wajibu wetu, ni jukumu letu kumuinua mbele za BWANA kwani kazi aliyoianzisha si nyepesi ni nzito, tumuinue mbele za BWANA kwa ajili yake, awe na afya njema, hekima, vilevile hata familia yake. vita aliyoianzisha. Vita aliyoanzisha ya uchumi ni kwaajili yetu sote. Sio kila mtu atafurahia hili jambo tunatakiwa kumuinua mtumishi huyu mbele za BWANA. Rais wetu Dkt. JP Magufuli anahofu ya Mungu sana, sasa kwanini tusitimize wajibu wetu? Nimekuwa nikisistiza kila mara napopata nafasi ya kusimama katika madhabahu hii, nikisema “tuliombee Taifa la Tanzania, Rais wetu, na hakika sasa mnaona mambo katika nchi yetu yanatimia. watu wengi wamegundua kuwa Rais wetu ni Nabii aliyetumwa na BWANA, ni mbeba maono wa Taifa la Tanzania. Taifa la Tanzania limebarikiwa kwa mbeba maono kutokana na yeye. Tanzania tuna neema, Mch. Noah Lukumay alisema, mataifa mengine yanatamani leo hii yanatamani kumpata Dr. John Pombe Joseph Magufuli kwenye nchi zao. Hakika ninahemewa kuiona Tanzania mpya chini ya Dr. John Pombe Joseph Magufuli, waliokuwa hawataki leo wanataka, kila iitwapo leo tupige goti kwa ajili ya Rais yetu mpendwa. Mungu awabariki, asanteni sana











Comments