Rev. Lucy Natasha kutoka Kenya amewasili jijini Dar es Salaam tayari kwa kongamano Kuu la Kumiliki na Kutawala kwa mwaka 2017 lililoanza katika kanisa la RGC Tabata Chang'ombe kwa Mtume Dkt. Peter Nyaga. Kongamano litaanza saa 9 alasiri hadi saa 2 usiku na kila siku kutakuwa na vipindi viwili, na mwisho wa kongamano hili ni tarehe 07.07.2017. Kutakuwa na waimbaji zaidi ya 13, na pia kutakuwa na wahubiri wengine kama Nabii Justin Mwingereza na Mtume Moses Mwakisunga.
Comments