RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

HIVI NDIVYO WATU WALIVYOMSIFU MUNGU KATIKA KANISA LA MLIMA WA MOTO MIKOCHENI "B"

TAFAKARI:

//ZABURI 102:1-3. Ee, BWANA, usikie kuomba kwangu, kilio changu kikufikie. Usinifiche uso wako siku ya shida yangu, unitegee sikio lako, siku niitapo unijibu upesi. Maana siku zangu zinatoweka kama moshi na mifupa yangu inateketea kama kinga.//

Hivi ndivyo watu wa Mungu walivyomsifu Mungu na kumuomba Mungu ili siku wa shida yao Mungu kusikia kilio chao na aweze kuwatetea ili wasiangamie na adui. Martha Komanya aliweza kuongoza kipindi cha kusifu na kuabudu siku ya Jumapili 18.03.2018 katika kanisa la Mlima wa Moto Mikocheni "B". Mhe. Bishop Dr. Gertrude Rwakatare aliungana na wana Mlima wa Moto Mikocheni "B" kumsifu Mungu kwa njia ya uimbaji na baadae walimtukuza Mungu kwa njia ya nyimbo za kuabudu amabzo ziliwapelekea kufanya maombi. Kila mtu aliwakilisha maombi yake kwa Mungu kulingana na kile alichokuwa anakihitaji Mungu amtendee.

Kama ulikosa ibada hii tunakualika katika ibada ya Jumapili hii saa 3 asubuhi hadi saa 8 mchana. Kanisa limendaa usafiri wa bure kuanzia kituo cha mabasi cha Makumbusho na Mwenge kwenye mataa barabara ya Coca Cola DSM

Martha Komanya





Mhe. Bishop Dr. Gertrude Rwakatare























Comments