MSIBA ULIOMKUMBA BLOGGER WENU WA RUMAAFRICA, RULEA SANGA ALIPOFIWA NA MAMA YAKE MZAZI AMBANGILE LANZON SANGA
Hii
ni siku ambayo siwezi kuisahau pale nilipompoteza mama yangu mzazi
katika hospitali ya Chimala Mbeya siku ya ya Jumamosi 22 Juni 2012.
Mama yangu alipata ugonjwa wa ghafla pale alipoaanza kutapika na baadae
kukimbizwa dispensary na baada ya kupimwa aligundulika ana malaria
mbili. Mama alirudishwa nyumbani na baada ya hapo usiku wake mama yangu
hali iliaanza kubadilika na kuishiwa nguvu. Hali hiyo ilizidi kuwa
mbaya na baadae kaka yangu Burton Sanga aliamua kukimbiza hospitali ya
Chimala iliyoko Mbeya. Mama aliaendelea na matibabu na baadae
kugundulika kuwa alikuwa na Blood Pressure (BP) na baada ya siku kama
mbili aligundulika kuwa anaumwa Kisukari. Siku tatu baadae hali ya mama
yangu ilikuwa mbaya sana.
Mama
aliwekewa mpira ya Oxygen na mrija wa kupitisha chakula. Mama hakuweza
kuongea kwa muda wote aliokuwa hospitali, lakini namshukuru sana Mungu
wangu, baada ya kuniona mama alicheka kicheko cha maumivu na kuniambia
"Mwanangu umekuja kuniuguza???" Nililia sana kumuona mama anavyoteseka
na kuhema, kwani alikuwa anasumbuliwa sana na utoaji na uingizaji
oxygen. Pia alikuwa analalamika na maumivu aliyokuwa anapata kutokana
na kulalia mgongo kwa muda mrefu.
Siku ya Jumatano mama yangu hakuweza kuongea kitu chochote, macho yake yalikuwa yamefumba na
mdomo wake ulikuwa umeachama kwaajili ya hewa. Mama alipochomwa na
sindano na daktari kama nne begani hakuweza kushtuka wala kuhisi maumivu
yote. Ndugu zangu walipokuwa wanatoa nguo zake mama alikuwa bado
kafumba macho yake na hakuonyesha sign ya kuumia.
Nakumbuka
kabla ya kifo cha mama yangu, ilikuwa ni siku ya Alhmaisi nilipomuombea
sana mama yangu na kuwaaga baadhi ya ndugu zangu kuwa nataka niende Dar
es Salaam kufuatilia pesa ambazo zitasaidia katika matibabu na siku ya
jumatatu nitarudi tena Mbeya kuumuuguza mama yangu, lakini
haikuwezekana. Ilipofika siku ya Ijumaa nilienda hospitalini kwaajili
ya kumuaga mama yangu na ndugu zangu kuwa naenda Dar.
Nilipofika
hospitalini nilikutana na shemeji yangu mke na kaka yangu Mchungaji
Burton Sanga, alinikimbilia na kuniuliza "begi lako liko wapi?" na mimi
nilimjibu "nimeliacha hotelini" aliniangalia kwa huruma sana, na mimi
nikaona baadhi ya ndugu zangu wako katika chumba cha kuhifadhia maiti.
Shemeji aliniambia "Jipe moyo mama hayupo tena duniani" nililia sana
kwa maana sikuamini kwani siku ya jana yake nilimuombea na kumshika
mkono, kumbe ilikuwa ndio alama ya kuaagana
Nilimshika mama yangu mkono kwa mara ya mwisho na usiku wa ijumaa mama aliaga dunia.
Siku
ya Ijumaa ya 22 Juni 2012 mida ya saa 4:30am mama aliaga dunia, na sasa
amepumzika katika makaburi yaliyoko Mbeya Uyole kama unaelekea Tukuyu.
Mama ameacha watoto wanne, Yohana Sanga, Fidness Sanga, Burton Sanga na Rulea Sanga.
Blogger
wenu nawaashukuru sana wale wote walionitumia pesa kwa kupitia Tigo
Pesa kama rambirambi na maneno ya faraja ambayo yalinifariji sana.
MUNGU WANGU ATAWALIPA
Ngoja tuone Safari nzima ilivyokuwa:
Nikiwa maeneo ya Morogoro
Mishika ndicho kilikuwa chakula changu siku hiyo
Nikisubiri safari kuanza kuelekea Mbeya
MAMA AKIWA KATIKA HOSPITALI YA CHIMALA MBEYA
Mama yangu Ambangile Lanzon Sanga akiwa amelazwa hospitalini Chimala Mbeya siku ya Jumamosi
Kutoka kushoto ni wauguzi, dada yangu Aulelia Mahenge mtoto wa mama mkubwa, Binamu yangu, Mama Simda
Shemeji yangu ambaye ni mke na kaka yangu Mchungaji Burton Sanga, Mama Judy.
Mama Judy amemlea mama yangu kwa muda wa miaka 17 tangia atoke Iringa na mpaka mauti imemchukua
Mama mdogo kulia akimuuguza dada yake pamoja na shemeji yangu mama Salome Sanga kushoto
Shemeji yangu mama salome akimsikiliza Daktari
Dada yangu Auleya Mahenge kutoka kwa mama mkubwa (kulia) akishikiria mkono wa mama yangu ili asichomoe mirija ya chakula na oxygen
Tukiwa nje ya hospitali tukisubiri kuruhusiwa kuingia hospitalini kuona mgonjwa
Kutoka kushoto ni mtoto wa kaka yangu mkubwa Yohana Sanga anayeitwa Christina Sanga, akifuatiwa na mke mtarajiwa wa kaka yangu Lusajano Sanga, mtoto mkuwa wa kaka yangu mkubwa Yoyaha Sanga, Salome Sanga, kaka yangu Burton Sanga ambaye alikuwa akimlea mama yangu kwa muda wa miaka 17, kaka mkubwa Yohana Sanga
Nikiwa katika harakati za kutafuta uji kwaajili ya mgonjwa (mamam yangu ambaye kwa sasa ni mamrehemu)
FAMILIA IKIMKARIBISHA SHEMEJI MTARAJIWA
Brother Burton Sanga kushoto akitambulisha
Dada Fidness Sanga akimkaribisha wifi yake mtarajiwa (wa tatu kutoka kulia) huku wakisubiria muda wa kwenda kumuona mgonjwa
MAREHEMU AMBANGILE LANZON SANGA, MZAZI WA BLOGGER RULEA SANGA
MAMA AKIWA KATIKA HOSPITALI YA CHIMALA MBEYA
Mama yangu Ambangile Lanzon Sanga akiwa amelazwa hospitalini Chimala Mbeya siku ya Jumamosi
Kutoka kushoto ni wauguzi, dada yangu Aulelia Mahenge mtoto wa mama mkubwa, Binamu yangu, Mama Simda
Shemeji yangu ambaye ni mke na kaka yangu Mchungaji Burton Sanga, Mama Judy.
Mama Judy amemlea mama yangu kwa muda wa miaka 17 tangia atoke Iringa na mpaka mauti imemchukua
Mama mdogo kulia akimuuguza dada yake pamoja na shemeji yangu mama Salome Sanga kushoto
Shemeji yangu mama salome akimsikiliza Daktari
Dada yangu Auleya Mahenge kutoka kwa mama mkubwa (kulia) akishikiria mkono wa mama yangu ili asichomoe mirija ya chakula na oxygen
Tukiwa nje ya hospitali tukisubiri kuruhusiwa kuingia hospitalini kuona mgonjwa
Kutoka kushoto ni mtoto wa kaka yangu mkubwa Yohana Sanga anayeitwa Christina Sanga, akifuatiwa na mke mtarajiwa wa kaka yangu Lusajano Sanga, mtoto mkuwa wa kaka yangu mkubwa Yoyaha Sanga, Salome Sanga, kaka yangu Burton Sanga ambaye alikuwa akimlea mama yangu kwa muda wa miaka 17, kaka mkubwa Yohana Sanga
Nikiwa katika harakati za kutafuta uji kwaajili ya mgonjwa (mamam yangu ambaye kwa sasa ni mamrehemu)
Brother Burton Sanga kushoto akitambulisha
Dada Fidness Sanga akimkaribisha wifi yake mtarajiwa (wa tatu kutoka kulia) huku wakisubiria muda wa kwenda kumuona mgonjwa
MAREHEMU AMBANGILE LANZON SANGA, MZAZI WA BLOGGER RULEA SANGA
Maiti ikiwa nyumbani kwake Uyole
Sanduku la maiti likipelekwa ndani ya chumba cha alichopumzika marehemu
Ndani ya jeneza
Jenezi likionyeshwa lilivyotengenezwa
Mwili wa marehemu Ambangile Sanga ndani ya Jeneza
MAZISHI YAKIFANYIKA KATIKA MAKABURI YA
UYOLE MBEYA
Umeumbwa kwa mavumbii utarudi mavumbi
Ndugu kutoka Makete wakiweka taji
Kaka na mke wake wakimsindikiza mama yao kwa kuweka taji
Kaka na shemeji wakimuaga mama yao mpenzi. Mama alikuwa anaishi na huyu kaka kwa muda wa miaka 17 Mbeya Uyole
Rulea Sanga, nikimuaga mama yangu kwa kumsindikiza kwa taji