RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

SWALI KWAKO MDAU WA BLOGU YA RUMAFRICA:
UNAJUA KUWA MAREHENU BOB MARLEY ALIMPOKEA YESU KRISTO KABLA YA KIFO CHAKE ?
Mtu mzima akisoma Biblia wakati wa uhai wake

Kuna watu wanampenda Bob Marley ama wanasema wanafuata nyayo au kuiga mfano wake, lakini ziko habari kwamba Bob Marley kabla hajafa alimpokea Bwana Yesu na kubatizwa kuwa muumini wa Orthodox na siyo Haile Selassie.

Bob Marley akiwa na mke wake Alpharita Constantia Anderson a.k.a Rita Maley Februari 10, 1966. 
Walibahatika kupata watoto watatu, lakini Bob Marley alimuoa Rita akiwa na watoto watatu kutoka kwa   kutoka kwa mume mwingine. Rita ana watoto 6 wakati Bob anao watatu

Cheti cha Bob Marley cha mazishi

Mzee akila good time

Alipokuwa katika mahojiano Askofu aliyembatiza Marley, Abuna Yesehaq wa kanisa la Ethiopia Orthodox, alisema Marley alikuwa mtoto wa Mungu tofauti na watu walivyomuona.
Aliendelea kusema “Ugonjwa wake wa kansa ulikuwa sababu kubwa ya yeye yeye kumpokea Bwana Yesu kama Bwana na mwokozi wa maisha yake. 
Akiwa michezoni..I wish angejiunga na Gospel Team ya Tanzania.

Watu wengi walidhani alibatizwa kwa sababu alijua angekufa, lakini haikuwa hivyo, alibatizwa kwasababu hakuwa na msukumo kutoka kwa yeyote na alipobatizwa aliikumbatia familia yake na kulia kwa nusu saa.”

Mzee kashikilia nini..unajua mwenzangu?

Marley alibatizwa tarehe 4 Novemba 1980 na alifariki 21 May 1981 akiwa na miaka 36.
Tukiachana na habari ya Robert Nesta Marley au Bob Marley, Kuna dini ya marastafari na washirika wake tunao mitaani ambapo kwa asilimia kubwa ni vijana, Je dini hii ya marasta wanaamini nini? na rasta zinahusiana vipi na kuvuta Bangi?


Rita Marley akiwa na watoto wake wakati wa mazishi 1981.

Comments