Samahani
wadau wangu wa Ruma Africa, leo ningependa kutoa ushuhuda wangu juu ya
matendo makuu ambayo Mungu ameyafanya kwangu tangia nimempokea Yesu
Kristo.
Kuna siku moja nilikuwa naagalia hizi picha zangu kabla sijampokea Yesu na mwokozi wangu, na nikawa natafakari maisha yangu ya badaae yatakuwaje. Nikiwa shule nilikuwa kijana mmoja mkorofi sana, na niliadhirika na maisha ya watu wa Marekani. Nilipenda sana kuishi kama mastaa wa Marekani hasa hawa waimbaji wa muziki wa Hip Hop. Nilikuwa napenda sana mavazi yao na ile kujifanya wagumu wasiojali wakubwa wala walimu wao.
Nakumbuka nikiwa kidato cha pili nilijiunga na kikundi fulani cha vijana waliofukuzwa shule ya Tambaza kutokana na utukutu. Nilipenda sana vile walivyokuwa wanafanya mambo yao ya kuwa kama gangstars. sikupenda kujishughulisha na masomo kiufasaha. Namshukuru Mungu hata kama sikuwa nafuatilia sana masomo, lakini kuna baadhi ya masomo nilikuwa nayaweza vizuri sana. Na jambo lingine Mungu aliniepusha na uvutaji sigara na ulevi, sikuoenda kabisa kusikia vitu kama hivyo maishani mwangu. Pia katika kundi hilo la tambaza hakuna aliyekuwa anavuta sigara wala pombe.
Nimesoma shule ya serikali ya Njombe inayoitwa NJOSS (Njombe Secondary School) kipindi hicho Mwalimu Mkuu alikuwa anaitwa Mwanyigu. Nikiwa shuleni hapo nilikuwa natoroka shule na kwenda disko. Na kurudi usiku wa manane shule na marafiki zangu. Kumbuka nilikuwa nasoma bweni. Mara nyingine nilikuwa nahonga pesa kwa viongozi wa bweni ili waweze kuniandika nilikuwepo bwenini wakati niko mjini-disko.
Nikiwa kidato cha nne nikaamua kumpokea Yesu Kristo kuwa mwokozi wa maisha yangu. Nikiwa shule kulikuwa na vikundi vya UKWATA, nilijiunga navyo na kuwa mtumishi mzuri sana. Niliendelea na wokovu huo mpaka sasa. Nikiwa katika wakovu kuna majaribu mengi niliyapata kutoka kwa rafiki zangu niliokuwa nashinda nao disko, walinicheka sana na kuniambia nimepotea sana. wasichana nilikuwa nao walinidharau sana, na wakasema siwezi kufika mbali na wokovu wangu.
Ni kitu gani kilinitokea baadae...Endelea kuvuatilia katika blogu hii, uone matendo makuu ya Mungu
BAADHI YA PICHA NIKIWA O'LEVEL NJOSS
Rulea wa pili kutoka kushoto nikiwa Mbeya kipindi cha likizo
Rulea Sanga niliyevaa sandos nikisoma bwenini
Rulea Sanga kushoto nikiwa na kikundi cha Tambaza. Kutoka kulia ni Allen Mwihava, wa tatu ni Nasoro, Tryphone na Embagise
Rulea sanga kulia nikiwa na rafiki yangu niliyempenda sana shuleni
Rulea sanga nikiwa na marafiki zangu, kulia ni Samy ambaye kwa sasa ameokoka, Yusuph
Nikiwa Disko
Rulea sanga katikati katika mapozi..Mungu anisaidie
Rulea sanga wa pili kutoka kushoto nikiwa na rafiki zangu Mbeya kipindi cha likizo
Rulea Sanga wa pili kushoto nikiwa na rafiki zangu wa kidato cha pili
Rulea Sanga wa tatu kutoka kushoto nikielekea mjini kuzurula wakati wenzangu wako darasani
Rulea Sanga wa pili kutoka kulia nikionyesha mapozi ya mamtoni, na rafiki zangu wa Tambaza
Kutoka kushoto ni Fikiri, Simon (niga), Deo ambaye alipata Division One, Rulea Sanga
Rulea Sanga wa pili kutoka kulia nikiwa na class mate zangu. Kulia ni Samy Black
Rulea Sanga kulia, nikiwa najisomea na rafiki yangu Fadhili Rwendo ambaye sasa hivi ni Mwanashera (Wakili)
Rulea sanga wa pili kutoka kushoto, wakati wa gradution yangu kidato cha nne
Rulea sanga nikiwa katika gari la Marehemu kaka yangu Amir Sanga maeneo ya Mafinga Iringa wakati wa likizo
Nikipata chakula cha jioni katika Dinning Hall NJOSS
Rulea Sanga wa tatu kutoka kushoto nikiwa na kundi la Tambaza
Rulea Sanga, kulia nikiwa na wadogo zangu wa kidato cha pili, wakati mimi nikiwa kidato cha tatu
Rafiki yangu Tryphone ambaye aliruka na Division One kidato cha nne wa kwanza kulia

Kikundi kutoka Tambaza
Rulea sanga wa pili kutoka kushoto nikiwa kidato cha pili na classmate wangu
Nikiwa kidato cha nne, niliyechuchumaa
ANGALIA PICH
ANGALIA PICH
Rafiki
yangu niliyempenda sana wa kitaa, anaitwa sebastian. Huyu jamaa alikuwa
kichwa sana Chuo Kikuu ila watu walimchezea akawa chizi. Ila kiingereza
usimguse
Nikiwa kanisani Mafinga kipindi cha likizo, niliyechuchumaa
Katikati ni Rulea sanga nikiwa na rafiki zangu, Tryphone (kushoto) na Sanjigwa
Nikiwa katikati na classmate, kushoto ni Onesmo Mhewa ambaye aligonga Division One kidato cha nne
Nikipiga Basketball































Comments