RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

PURE MISSION KUWAWEKA VIJANA WA KIKRISTO KATIKA HALI YA KUJITAMBUA

Fredy Msungu siku ya leo alitembelea ofisi za Rumafrica kwaajili ya kutambulisha project yake na Angel Benard inayoitwa “Pure Mission”. Pia alisema kuna watu 15 waofanya nao kazi na wengine wako mikoni na  vyuoni kama vile chuo cha Mzumbe Morogoro, Tumaini Iringa, UD na vingine vingi.

Alisema, lengo kuu la project kuwaweka vijana tayari katika kupambana na changamoto nyingi zinazowakabili vijana wa Kikristo Tanzania. Pure Mission inawalenga vijana wa kizazi kipya kuwa bora hasa kwa wale watakaoshika vitengo nyeti serikalini na makampuni ya watu binafsi

Vitu vinavyofanyika katika Pure Mission ni Talk Show, Movement mbalimbali kwa vijana, Praise and Worship, Motivation kwa vijana walioko mashuleni na vyuoni,

Fred alimshukuru Mungu kwa kuwawezesha kwa kazi hii ambayo wanayofanya kwaajili ya vijana.

Pure Mission huwa inafanya matamasha makubwa matatu kwa mwaka, mwanzoni mwa mwaka, katikati mwa mwaka na mwishoni mwa mwaka. Na sasa wako mwisho wa mwaka kwahiyo kuna tamasha limeandaliwa mkoani Iringa ambapo tarehe 19 Octoba 2012 watakuwa katika Chuo cha Tumaini, tarehe 20 Octoba watakuwa Chuo cha RUCO na tarehe 21 Octoba 2012 kutakuwa na Shout of Joy Concert ukumbi wa Highland Hall kuanzia saa 9:00 Mchana – 3:00 usiku.

Mengine mnaweza kusikiliza katika clip hiyo hapo chini, ni memgi yamezungumziwa:
 Fredy Msungu ndani ya ofisi za Rumafrica





Comments