RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

OBAMA SASA AITWA 'BWANA NA MWOKOZI'


Mshindi wa tuzo ya sanaa ya Academy Awards, (tuzo za Oscar) Jamie Foxx, ameibuka hadharani na kudai kuwa Rais Obama ni Bwana na Mwokozi wao, katika tukio la kutoa tuzo la Soul Train Awards mjini Las Vegas, Marekani.
"Ni kama kanisa hapa, yaani ni kama kanisa humu. Kwanza kabisa, tumpe heshima Mungu na Baba yetu, Mwokozi Barrack Obama, Barrack Obama" alisema Foxx na kushangiliwa na umati wa watu uliokuwa ukimsikiliza kwenye tukio hili la jumapili usiku.
Kufuatia tukio hilo na kuenea kwa habari, kimemfanya kiongozi wa muunganiko wa Kanisa katoliki kwa ajili ya dini na haki za binadamu, (Catholic League for Religious Civil Rights) ambaye amekuwa mpinzani wa baadhi ya sera za Rais Barrack Obama, ikiwemo ile ya sera ya afya ya kupandikizwa 'microchip' kuwa ni ya kushangaza.
"Licha ya kwamba Obama ameshindwa kuzuia bahari zisijae (kama alivyoahidi mwaka 2008) bado amefanikiwa kumshawishi Jamie Foxx, na sina shaka baadhi ya wafuasi pia, kuwa Mungu yupo. Ijapokuwa Mungu anaweza kuchoropoka kesi ya ACLU (muunganiko wa vyama vya kiraia nchini Marekani vinavyotetea haki za binadamu) dhidi yake kwa kumtuhumu kulitenda kanisa ndivyo sivyo, na haki kutopatikana"
Kiongozi huyo (Bill Donohue) pia amekumbushia mwaka 2011 ambapo Foxx aliulizwa katika mahojiano kuwa Mungu anamaanisha nini kwake, na yeye akajibu kuwa hajui. Tazama video yake.


Mapema mwaka huu, uongozi huo wa kikatoliki ulimuandikia Rais Obama barua, ikiainisha mambo mbalimbali ambayo Obama husita kufanya ama kuzungumza kuhusu Mungu.
"Suala ni kwamba Obama hayuko sawasawa na urithi wa kikristo wa Wamarekani, hata mwaka 2010 hakuweza kutamka wazi maneno 'In God We Trust', wakati akizungumzia msemo wa taifa letu nchini Indonesia, badala yake akasema 'E Pluribus Unum' yaani yeye anaridhika na upagani." Donohue alisema.

"E Pluribus Unum = Kilatini. wamoja kutokana na wengi (One out of many) Maneno haya yapo kwenye fedha za Marekani yakimaanisha kuwa wao ni kitu kimoja kilichotokana na wengi."
Kwenye kipindi cha uchaguzi mkuu,Obama alitengeneza video kadhaa na tovuti ya taarifa ambapo alikuwa akijibu maswali ya wananchi moja kwa moja kuhusiana na imani yake, akiuhakikishia umma wa Wamarekani kuwa yeye ni mkristo safi, anayeomba mara kwa mara na huweza kupigania uhuru wa dini nchini humo.

Comments