RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

NABII FLORA: UJUMBE WA TAREHE 22.02.2013: BWANA ATAFANIKISHA NJIA ZAKO



Tutasoma kitabu cha Mwanzo 24:55-58 (Ninakuomba usome Biblia yako), name nitakwenda kufafanua kama ifuatavyo:

Mwambie msichana mwenzako ambaye hajaolewa kuwa huu ni wakati wa kuondoka na Yule umpendae, huu ni wakati wa Bwana. Huu ni wakati wa Bwana wa kukupa mume aum mke umpendae sasa, asema Bwana wa majeshi. Ni wakati wa Bwana kukupa haja ya moyo wako, asema Bwana wa majeshi..Amen!!
Maadamu Bwana amefanikisha njia zako, ninasema lazima Mungu atakwenda kufanikisha njia zako Octavian, na Bwana atafanya kama moyo wako unavyohitaji.

Asubuhi ya leo, tupo hapa ili Bwana apate kufanikisha njia zetu, na atafanikisha njia zako zote ili uweze kufanikiwa. Kwani huwezi kuoa kama Bwana hajafanikisha njia zako, Kama bwana hajafanikisha njia zako huwezi kupata mwenzi wa maisha. Bwana atakapo fanikisha njia zako, ndipo utamwambia Bwana naomba nitokeze..haleluya!!.
Usikimbilie ovyo katika suala la kuoa na kuolewa, kuna watu wengi wamekuwa wakijinyonga, kwasababu ya kuruhusu Yule ampendae kwa kuwa Bwana amefanikisha njia. Unaruhusu Yule umpendae, wakati wengine wanazuia na kusema hakuna kuondoka, na mwisho wake utakuta watu wanameza vidonge.
Wewe binti unavyotaka kuondoka na huyu kijana, Je, unamtambua?
Mama yangu ninaomba Mungu afanikishe watoto wako waolewe wiki hii. Mungu afanikishe njia zako mama watoto wako wafunge ndoa, Mungu akufanikishe njia za watoto wako, Bwana afanikishe njia za uzao wako. Umekuwa ukichangia michango ya wenzako, mwaka huu Mungu akufanikishe wachangie kwako. Mwaka huu mwambie Bwana afanikishe njia zako mama.

Nabii Flora akifundisha Neno la Mungu

Ninaona mama Mungu anenda kufanikisha njia zako. Ninaomba Bwana atende muujiza kwako, Bwana afanikishe njia zako. Pokea mama, umefika mwisho wa kuchangia michango ya watu wengine. Watu waliokuona huolewi waone ukiolewa, na sisi lazima tukushangilie. Ninasema lazima Bwana akufanikishe njia zako leo, ninasema akina mama mnaenda kufanikisha njia zenu. Sema “Bwana anaenda kunifanikisha njia zangu leo”.
Na huko uendako, Bwana atakwenda kukufanikisha, atakufanikisha hata katika malango ya wanaokuchukia.

Bwana atakufanikisha njia zako na kukuwezesha kumiliki mashamba, walisema hutaolewa utaenda kuolewa, nasema lazima Bwana akufanikishe njia zako, na utaenda kumiliki malango ya adui zako, Atakaye kuleta mbele zako kukuzuia, Bwana atakusogeza mbele. Unajua katika suala la kuoa au kuolewa, kuna maadui yanazuia Baraka. Watu wanaanza kusema Yule mwanamke ni ‘Kiwembe”, “wafanyabiashara wengi wametembea naye”, wanakuaharibia siafa ili wewe Bwana asiende kufanikisha njia zako, alikini asubuhi ya leo Bwana asema, anaweka uzibe mbele yako, Bwana atamtoa. Mungu atakufanisha njia zako asubuhi ya leo, ninapenda kukuambia kuwa Bwana ataenda kufanikisha njia zako leo, utaenda kuona na kuwa mama wa mataifa mengi na utamiliki milango yao.
 Mafundisho yakiendelea na nabii Flora


Mwanandoa, bwana atafanikisha mambo yako, watoto wako wataolewa, binti mwaka huu Bwana ankwenda kufanikisha njia zako. Ninajua kabisa mchumba uliyenaye hakutaki, unaona haeleweki, Mungu atakupa mume mzuri kutoka Afrika Kusini atakuoa wewe, tena mtanashati, na mwenye hadhi yake, Mungu atakuletea kijana mzuri kutoka Uingereza, utakuletea kijana mzuri kutoka Italy, atakupa na atakuja kwako kutoka Marekani, atakufanikishia njia zako, asema Bwana
Mwaka huu ni mwaka ambao Bwana anenda kubadiliusha njia zenu. Ninawambia ndugu zangu na vijana, mliofungwa, mwambie Bwana aafanikishe njia zangu.  Naomba kuona vijana wanaotaka kuoa na kuolewa mmwambie Bwana afanikishe njia zako mwaka huu, natarajia kupata mwezi huu hata mwaka usiishe. Munaetaka Bwana awape waume na wanawake nyoosheni mikono na Mungu ataenda kufanikisha njia zako, asema Bwana wa majeshi.
Atakaye kuwa mbele yako kukuzuia muujiza wako, Bwana atakwenda kumuondoa, Mungu wangu atakwenda kumuondoa mbele yako
Tusome katika kitabu cha Isaya 34:24:16. Hapana hata mmoja atakosa mwenzake. Utaenda kujisomea mwenyewe.


KIPINDI CHA MAOMBI
tutakwenda kusoma katika kitabu cha Mathayo 3:1 (Naomba ujisomee na mimi nitafafanua kama msomaji wangu atakapokuwa anasoma)
Yohana Mbatizaji alikwenda kuhubiri huku na kule, kuhubiri habari njema za Mungu, akisema tubuni tubuni kwa maana ufalme wa Mungu umekaribia, kwababu huyu ndiye aliyenenwa habari zake na Nabii Isaya akisema, “sauti ya mtu aliyae nyikani.
Hata sisi hapa tunashida tunamlilia Bwana usiku na mchana. Usiku tunamwita Bwana aka ile sauti ya mtu aliyae nyikani. Ninasema nikilia lazima watu waweze kufunguliwa, kupona kansa, tunalia ili jamii kuwa na amani, taifa kuwa na amani, tunalia ili Bwana aweze kuponya taifa letu.
Ninakuambia mama hii ni sauti ya mtu aliyae nyikani, ninalia kansa ionsdoke kwako, kichaa kikuepuke, njaa ikuepuke, watu wanaochechea wawe sawa. Hii nisauti ambayo Bwana anaihitaji.

Bwana anasema itengenezeni njia ya Bwana, yanyoosheni mapito yake. Na sisi tunakwenda kunyoosha mapito Yake, Bwana atakuinua katika kiwango kingine. Ukisoma Methali 3:5, anasema, yanyooseheni mapito yake, yaani ukinyoosha haya mapito yake Bwana atapita kwako, atapita kwa Jeremia, atabadilisha mapito yako. Inawezekana leo.
Nabii Flora kushoto akiwa na dada ambaye alikuwa akitolea mfano juu ya kuolewa
 Mungu humtumia Nabii Flora kukuletea ujumbe wa Mungu kama ulivyo..
Andika Methali 3:24. Hapa anasema hii nisauti ya mtu aliyenikani, itengenezeni njia ya Bwana, yaani yanyoosheni mapito yenu, nyoosheni mioyo yenu ili Bwana aweze kupita. Mama na Baba anagalia moyo wako, takasa moyo wako maana Bwana anataka kupita, Mungu anahitaji wewe kufungua moyo wako asubuhi ya leo ili Bwana aingia ndani yako.


Kwasababu yako wewe mpendwa unayempenda Bwana, unatumia nauli yako huko ulikotoaka kuja mahali hapa. Na mimi nasema sitanyamaza kukuombea kwa Mungu Baraka, sitanyaza kukutamkia mema, sitatulia mpaka upate ajira, sitatulia mpaka umefanikiwa, sitatulia mapaka umekuwa na amani. Mpaka nione matokeo kwako mama na wewe baba.
Unapitia mateso, yuko Mungu atakayekufanikisha siku ya leo, na mimi nasema sitanyamaza wala sitatulia mpaka haki yako imetokea, mpaka ndoa yako imekuwa na amani,  mpaka umefanikiwa kwenda Ulaya, sitatulia Gideon Mutalemwa mpaka albamu yako imevuma Tanzania nzima.
Nitalia na wanaolia, nitafurahi nao wanaofurahi. Mama hutalia peke yako, nitamlilia Mungu, ukoo umekutenga, jamii imekutenga, watu wamekuchukia bila sababu,. Ninahitaji Mungu akutendee Baba, Bwana atakufanikisha utafanikiwa katika njia zako wewe!!!

 Wa pili kutoka kushoto ni dada Mtanzania anayeishi nchini UTURUKI ambaye alikuja kwa Nabii Flora kuombewa kutokana na tatizo lake la kuchanganyikiwa
 Watu wakitafakari kwa amkini Neno la Mungu linalofundishwa na Nabii Flora
 Baadhi ya waumini waliopita mbele baada ya kuitwa na Nabii Flora kwaajili ya mifano
 Mikono ikiwa imeinuliwa kama ishara ya kusarenda kwa Yesu.
 Maombezi yakiendelea
 Nabii Flora akiwaonysha watu wa Mungu Tshirts mpya za Kanisa. Na akiwasisitiza kununua. Tshirts hizi zimetengenezwa na RUMAFRICA


Octavian
 Nabii Flora akifundisha Neno la Mungu
 Nabii Flora akihakikisha neno la Mungu alilopewa kwaajili ya watu likiwafikia


 Dada akitoa ushuhuda wake
Shuhuda zikiendelea

Mwandishi
Rulea Sanga wa www.rumaafrica.blogspot.com au simu +255 715851523
Mpiga Picha ni Octavian wa Kanisa la Nabii Flora

Comments