RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

MUUAJI WA PADRI EVARIST MUSHI AKAMATWA.



MTU anayesadikiwa kuwa ndiye Muuaji wa Padri Evarist Mushi wa Kanisa Katoliki Mjini Zanzibar, amekamatwa alasiri hii Maeneo ya Kariakoo Zanzibar.

Jeshi la Polisi limethibitisha kukamatwa kwa Mtuhumiwa huyo na kwenda nae kituoni kwa ajili ya Mahojiano zaidi.
Padri Evarist Mushi aliuawa Mwezi uliopita kwa kupigwa risasi akiwa kwenye gari lake kuelekea Kanisani kwenye Ibada ya Jumapili.
Tutakupasha habari kamili pindi zitakapotufikia. Endelea kutembelea Mtandao huu.

- Issa Michuzi -

Comments