RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

18.06.2017: ASKOFU JOSEPHAT MAKONGORO WA KANISA LA EFATHA MWENGE DSM AMSHUKURU BISHOP DR. GERTRUDE RWAKATARE KWA MAONO YA KUMUOMBEA RAIS NA TAIFA LA TANZANIA DKT. GERTRUDE RWAKATARE...

Siku ya Jumapili 18.06.2017 Askofu  Josephate Makongoro alikuwa na haya ya kusema, wa Bwana Yesu asifiwe. Ninashukuru Mungu kufika hapa Mlima wa Moto Mikocheni “B”, mimi natokea kanisa la Efatha Ministry Mwenge kwa Nabii Josephate Mwingila, imenipendeza leo kuwa pamoja na ninyi Mlima wa Moto kuungana na mama yetu Bishop Dr. Gertrude Rwakatare kwa kumuunga mkono kwa maombi ya kumuombea Rais wetu Mh. Dr. John Pombe Magufuli katika kampeni hii ya kutokomeza umaskini hapa Tanzania kwa maana watu wametudhurumu mali zetu muda mrefu sana,  basi kwa mikono miwili tunaomba tum-”surpot” mama yetu kunamuombea Rais wetu. Pia tuviombea vyombo vyote vya serikali kwani vinafanya kazi pamoja na Rais wetu kwa umakini pamoja na Bunge, mahakama na polisi. Lakini pia tunamshukuru Mungu kwa sababu mama yetu anamaono makubwa katika jamii ya Watanzania. Tuko kwenye kipindi cha mwisho, Yesu yu karibu kurudi, nawapenda Mungu awabariki, Efatha inawapenda pia.

//Bishop Dr. Gertrude Rwakatare//
//Mlima wa Moto Mikocheni "B"//
//Ibada ya Jumapili hii ni saa 3 asubuhi - saa 8 mchana//
//Usafiri ni bure kuanzia kituo cha mabasi cha Makumbusho au Mwenge kwenye mataa barabara ya Coca Cola, utaona magari yetu//