RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

SISI MAWAZIRI HATUNG'OKI-PINDA
Waandishi Wetu
WAKATI madaktari wakisisitiza kufanya mgomo waliouita wa kihistoria kuanzia leo kushinikiza kuondolewa madarakani kwa Waziri wa Afya, Dk Haji Mponda na Naibu wake, Dk Lucy Nkya, Waziri Mkuu, Mizengo Pinda amewasihi wataalamu hao wa afya kutochukua hatua hiyo kama kweli wana nia ya dhati ya kuwasaidia wananchi.

Jana, madaktari hao walibandika mabango katika Hospitali ya Taifa Muhimbili wakisisitiza kuanza mgomo huo leo hali ambayo imezua kutaharuki kubwa miongoni mwa wagonjwa na jamaa zao. Muhimbili ndiko kulikokuwa chimbuko la mgomo wa madaktari uliofanyika mwezi uliopita.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Dar es Salaam jana, Waziri mkuu Pinda alisema Serikali haioni sababu ya kuwawajibisha mawaziri hao kwa sasa na kueleza kushangazwa kwake na hatua ya madaktari hao kugeuza suala hilo kuwa dai namba moja hivi sasa.

“Hivi kweli mnataka nifike mahali nimwaambie Rais (Jakaya Kikwete) tunakupa saa 72 uwafukuze kazi viongozi hao? Hapana... hapana... hapana kwa lipi hasa? Siwezi kumwambia atekeleze hayo. Ingekuwa hatujafanya chochote sawa, hata angekuwa mtu yeyote hawezi kukubalina na hayo unless (vinginevyo) wenzetu madaktari watuambie wana hoja nyingine.”

Pinda alisema Dk Mponda mwenyewe anayelalamikiwa ndiyo kwanza ana mwaka mmoja na nusu kazini na hata madai mengine hayajui kwa kuwa hakuwepo wakati huo akisema shinikizo la kutaka awajibishwe ni kumuonea.

Alipoulizwa endapo mawaziri hao wataamua kuwajibika wenyewe ili kunusuru maisha ya Watanzania Serikali itakuwa tayari kwa hilo, Pinda alihoji: “Kwa lipi hasa? Naona ni vyema tusubiri majadiliano, hayo yote yatajulikana baada ya kufikia mwisho.”

Waziri Mkuu aliwataka madaktari kutumia busara, hekima na uzalendo na kuendelea na kazi kama kawaida wakati Serikali inaendelea na majadiliano na viongozi wao.

“Nawapa rai ndugu zetu madaktari wasigome kama wanavyodhamiria kufanya kwa sababu watawaumiza watu wasio na hatia, turudi tuweze kukamilisha majadiliano tuliyoyaanza,” alisema Pinda.

Alipoulizwa kuhusu hatua ambazo Serikali itachukua endapo madaktari hao watagoma leo alijibu: “Tuache tuone, tukiamka asubuhi (leo) kama ni ngangari itabidi sisi kama Serikali tutaangalie cha kufanya.”

Alisema sheria imeweka bayana kuwa watu wanaotoa huduma katika maeno nyeti hawapaswi kugoma kwa kuwa kufanya hivyo wanahatarisha usalama, afya na maisha ya watu.

Alizitaja huduma hizo muhimu kuwa ni pamoja na maji na usafi, umeme, afya na maabara, zimamoto, udhibiti wa safari za anga na mawasiliano ya ndege za kiraia na huduma yoyote ya usafiri inayohitajika kwa ajili ya kutoa huduma hizo.
“Migomo iwe ni ya wafanyakazi au waajiri, iwe ni batili au halali ina athari kubwa sana kwa ustawi wa jamii na maendeleo ya taifa kwa ujumla endapo itatekelezwa,” alisema.

Pinda alisema kutokana na ukweli huo, ndiyo maana sheria za kazi zimeweka mifumo na taratibu za kutatua migogoro ya kikazi kabla haijazaa migomo. Alisema Sheria ya Ajira na Uhusiano Kazini Na. 6/2004 na ile ya Utumishi wa Umma Na. 8/2006 zinatambua haki ya wafanyakazi na waajiri kugoma lakini baada ya utaratibu ulioinishwa kuzingatiwa vinginevyo migomo hiyo itakuwa batili.

Alitoa mfano wa Kifugu cha 80 (1) cha Sheria ya Ajira na Uhusiano Kazini Na. 6/2004 kuwa mgomo halali ni ule ambao mgogoro wake ni maslahi, umejazwa kwenye fomu maalumu na kuwasilishwa katika Tume ya Usuluhishi na Uamuzi, haujasuluhishwa katika kipindi cha siku 30 tangu ulipopokewa na Tume au katika kipindi alichoongeza msuluhishi.

Alisema mgomo unaoitishwa na madaktari hao pamoja na kuwa ni wa kimaslahi, haujawahi kuwasilishwa kwenye tume aliyoitaja kwa usuluhishi na pia haujaitishwa kwa mujibu wa sheria hiyo ya ajira.

Utekelezaji wa madai 
Akizungumzia utekelezaji wa madai ya madaktari hao, Waziri Mkuu Pinda alisema Serikali imekuwa ikiyatekeleza akitolea mfano hatua yake ya kuahirisha safari ya kwenda Dodoma kwa saa kadhaa ili aweze kuonana nao na kusikiliza madai yao.
Alisema madai ya kurudishwa kwa madaktari walio katika mafunzo Muhimbili yametekelezwa kama ilivyokuwa katika madai ya kuongezwa posho.
Kuhusu kubadili uongozi wa juu wa wizara, Pinda alisema aliwaeleza kwamba suala hilo liko mikononi kwa Rais ambaye ndiye mwenye mamlaka ya uteuzi wao.

Akizungumzia madai mapya, Pinda alisema wakati Serikali ikishughulikia madai yao, madaktari wamekuja na sharti jipya la kutaka uongozi wa juu wa wizara uondolewe ndipo majadiliano yaendelee.

“Serikali inajiuliza kama kweli madaktari wana nia ya dhati ya kumaliza matatizo yao au wana ajenda nyingine ambayo sisi kama Serikali hatuifahamu?,” alihoji.

Alisema ameshangaa kuona.... Soma zaidi: http://www.mwananchi.co.tz

Comments