RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

FLORA MBASHA AREJEA NCHINI AKITOKEA MAREKANI, KUIMBA KWENYE MKUTANO JANGWANI

Flora Mbasha akiimba kwahisia katika moja ya tukio nchini Marekani.                   
Baada ya ziara ndefu huko nchini Marekani mwimbaji nyota wa gospel nchini Flora Mbasha pamoja na mumewe wamerejea nchini. Waimbaji hao walikwenda nchini Marekani toka mwezi March mwaka huu na kufanikiwa kuimba katika makanisa na mikusanyiko ya watu wa Mungu pamoja na semina ya mwalimu Christopher Mwakasege.''

Wall



  • Bwana Yesu asifiwe sana. napenda kuwashukuru wote kwa maombi yenu na ushirikiano wenu kwa kipindi chote tulichokuwa Marekani kwenye huduma, sasa tumerudi Tanzania salama kabisa. Mungu awabariki sana tunawapenda naomba tuzidi kuwasiliana, kushauriana na kutiana moyo katika safari yetu ya kwenda mbinguni. Amen

Pia waliweza kutembelea ubalozi wa Tanzania nchini Marekani na kukutana na watanzania wanaoishi nchini humo, Flora Mbasha anayetamba na matoleo mbalimbali ya muziki aliweza kujitambulisha vyema katika tasnia hiyo alipotoa wimbo Tanzania uliotoa hamasa kwa waimbaji wengine zikiwemo kwaya kuimba juu ya Tanzania, pia wimbo wa Jipe moyo,Kila jambo,Yatima, wimbo wa maisha ya ndoa aliomshirikisha mumewe Emmanuel Mbasha pamoja na wimbo wenye mahadhi ya watu wa mikoa ya Pwani uitwao Mwanamke simama imara.

Kwasasa mwimbaji huyo anamiliki studio yake mwenyewe ya kurekodia iliyopo Tabata anakoishi pamoja na kuwa na matoleo ya audio na video zaidi ya mbili, mwimbaji huyu ni mmoja kati ya waimbaji wanaomtukuza Mungu katika mkutano mkubwa wa injili uitwao June Crusade unaoendelea katika viwanja vya Jangwani jijini Dar es salaam ukitarajiwa kuhitimika jumapili hii huku mnenaji mkubwa akiwa ni askofu mkuu wa E.A.GT. Dkt. Moses Kulola ambaye ni babu wa mwimbaji huyo. Karibu nyumbani Flora na Emmanuel Mbasha asanteni kwa kutuwakilisha unyamwezeni.



           ANGALIA BAADHI YA PICHA ZA MATUKIO YAO NCHINI MAREKANI


Walitembelea Sauti ya America kitengo cha Kiswahili kama unavyowaona.


Akiwa na balozi Mh. Mwanaidi Majaar alipomtembelea ofisini kwake.
Story zikiwa zimenoga mwe
Mbasha akitoa darasa la kucheza mwe style ya pikipiki kama sio baiskeli.
Weee Mbasha wewe haya tuambie hiyo ni key gani mwe


Flora aliweza kusherehekea sikukuu yake ya kuzaliwa nchini Marekani, hapa akiwa na keki yake.

Comments