WAIMBAJI WA ''KWETU PAZURI'' KUTUA UWANJA WA NDEGE JIJINI DAR ES SALAAM ALASIRI HII
Sarah Uwera mmoja wa waimbaji wa kundi hilo, walipotembelea nchini mwaka jana. |
Kundi la kwanza la kwaya hiyo liliondoka jana kwa njia ya basi kuja jijini, huku kundi la pili ndio litawasili kwa ndege mchana wa leo.
Hii itakuwa mara ya nne kwa waimbaji hao kufika nchini ambako wamekuwa na mashabiki lukuki, kutokana na uimbaji wao, ambapo safari hii wanatarajia kuwepo kwa wiki nzima jijini Dar es salaam ikiwa maalumu kwa mkutano huo,Pia wanatarajia kuwasili na toleo lao jipya la kanda ambalo baadhi ya nyimbo zimeanza kusikika katika vituo vya radio kama Wapo Radio Fm pamoja na Morning Star radio zote za jijini hapa.
Kanda mpya ya Ambassadors of Christ Rwanda. |
Comments