Siku ya jumamosi jijini London nchini Uingereza kumefanyika tukio kubwa
la utolewaji wa tuzo za Africa Gospel Music Awards(AGMA) 2012, tukio
hilo ambalo watanzania wengi walikuwa na matarajio ya kuona mwimbaji wao
pekee aliyependekezwa kuwania tuzo hizo katika vipengele viwili
kushindwa kupata tuzo hizo kutokana na kura alizopigiwa kuwa chache
hivyo kuwapa mwanya waimbaji wengine aliokuwa akiwania tuzo hizo
kuondoka na tuzo hizo, bofya hapa kujua washindi.
Onyesho hilo ambalo lilianza kwa kupooza kutokana na watu kuchelewa
kuanza kuingia ukumbini pia asilimia kubwa ya watu hata walipoingia
ukumbi huo ulio chini ya El shaddai Christian Centre waimbaji waliokuwa
wakiimba hawakuweza kuwafanya watu hao wasimame zaidi ya kufurahia
huduma yao kwa kuwapigia makofi mara walipomaliza kuimba. Shughuli hiyo
ambayo iliongozwa na washereheshaji (MC) wapatao wanne wakiwemo waimbaji
kama Diana Hamilton, Rebecca, Wole Awola na mwenzao ambaye ni
mchekeshaji aliyeweza kuwavunja mbavu kwa vicheko kutokana na lafudhi na
vichekesho hivyo kuwahusu hasa watu kutoka Afrika magharibi ambao
walikuwa wameujaza ukumbi huo.
Mwanadada Emmy Kosgei kutoka nchini Kenya ambaye usiku huo alijishindia
wimbo bora wa mwaka ndiye aliweza kusimamisha watu waliokuwepo ukumbini
hapo kwa jinsi alivyoweza kuimba kwa ustadi nyimbo zake mbili ukiwemo
Ololo ambazo kila wimbo aliimba kwanza kwa CD kisha wanamuziki
waliokuwepo kuendeleza live mara ulipoisha kwakuwa hawakuweza kufanya
mazoezi kabla, mwimbaji huyo aliweza kuwa nyota usiku huo kwani baada ya
tamasha nusu ya watu walioujaza ukumbi huo walimzunguka kutaka kupiga
picha naye pamoja na kuchukua mawasiliano yake.
Kundi la Makoma ambalo halikuweza kupata tuzo yoyote usiku huo
halikuweza kufika ukumbini hapo kwa wakati kutokana na taarifa
zilizopatikana baadaye kwamba walipata ajali wakiwa njiani kuja ukumbini
hapo ndio maana hawakufika ingawa walituma meneja wao pamoja na mmoja
wa waimbaji wa kundi hilo ambaye alipozungumza na GK akasema Makoma wapo
vizuri, Mungu akipenda wanapanga kuja Tanzania mwakani.
ANGALIA BAADHI YA PICHA AMBAZO GK ILIZIKUSANYA SIKU YA TUKIO
Comments