RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

CHEMSHA BONGO NA BIBLE

Mtungaji wa Maswali: Rulea Sanga

CHEMSHA BONGO
Inatusaidie wewe na mimi kuijua Biblia na kumpenda Kristo. Nitakuwa nauliza maswali katika kitabu  fulani, kwa mfano mwezi huu wa Julai tutakuwa tunaulizana maswali katika kitabu cha MATHAYO na mwezi unaofuta itakuwa kutoka katika kitabu kingine.

Rulea Sanga

NB: Naomba usiangalie majibu kabla hujajibu kutoka katika akili yako:

SEHEMU YA TISA
KESHO KUTAKUWA NA MTIHANI WA MWISHO WA MWEZI. JIANDAE MTUMISHI WA MUNGU. NAKUTAKIA MAANDALIZI MEMA

MASWALI
1.      Ni ishara gani alifanya yule aliyemsaliti Yesu (Yuda), kwa wale makuhani na lile kundi kubwa lililokuja kumkamata Bwana Yesu?

2.      Ni nani aliyekatwa na yule aliongozana na Yesu wakati kipindi cha kusalitiwa Yesu kilipokaribia?

3.      Ni siku gani ambayo Yesu alisema ataenda kusalitiwa na makuhani, na wazee na watu watakusanyika katika behewa Kuhani Mkuu jina lake Kayafa?

4.      Unafikiri ni kwanini Yesu hakukamatwa kwa hila ya kmwua ile siku ya Pasaka?

5.      (i) Taja majina mawili ya watu ambao Yesu aliwashika na kuanza kuhuzunika na kusononeka, na akawambia wale waliokuwa Naye, “Roho yangu inahuzuni nyingi kiasi cha kufa, kaeni hapa mkeshe pamoja nami”.

(ii) Yesu aliombaje, baada ya kusema “Roho yangu inahuzuni nyingi kiasi cha kufa, kaeni hapa mkeshe pamoja nami”?

(iii) Kwanini Yesu alitamka maneno haya, “Kesheni, mwombe, msije mkaingia majaribuni, roho i radhi, lakini mwili ni dhaifu”

(iv) Je Yesu aliweza kuomba tena mara ya pili baada ya kuwambia wanafunzi wake wakeshe na kuomba?

(v) Yesu baada ya kurudi tena kuomba, aliwakuta wanafunzi wake wamelala au wanaomba?

(vi) Ni mara ya ngapi Yesu aliomba na kuwambia wanafunzi wake, “Laleni sasa, mpumzike, tazama saa imekaribia, na mwana wa Adamu anatiwa katika mikonoya wenye dhambi”?

6.      Wakuu wa Makuhani wote na wazee na watu wakafanya shauri juu ya Yesu, wapate kumwua, wakamfunga, wakamchukua, wakapmpelekea nani?

7.      (i) Yuda alipoona ya kuwa Ysu amekwisha kuhukumiwa, alifanya nini?

(ii) Ni maneno gani Yuda alisema baada ya kurudisha vile vipande alivyopewa kwaajili ya kumsaliti Yesu?

(ii) Yuda baada ya kukimbia ndani ya hekalu kutokana na kumsaliti Yesu alifanya nini?

8.      (i) Yesu alipovuliwa nguo zake na askari wa liwali kwajili ya kusulubiwa, alivalishwa nguo ya rangi gani?

(ii) Taja baadhi ya mateso aliyopata Yesu baada ya kuvuliwa nguo zake na kuvishwa nguo nyekundu.


MAJIBU
1.      Alimbusu (Mathayo 26:48)

2.      Mtumwa waKuhani Mkuu, Kayafa (Mathayo 26:51)

3.      Baada ya siku mbili itakuwa Pasaka (Mathayo 26:2)

4.      Waliogopa isije ikatokea ghasia katika watu (Mathayo 26:5)

5.      (i) Petro na wana wawili wa Zebedayo (Mathayo 26:37)

(ii) Alienda mbele na kuanguka kifulifuli akiomba akisema “Baba yangu ikiwezekana kikombe hiki kiniepuke, lakini sio kama nitakvyo mimi, bali kama utakavyo wewe” (Mathayo 26:39)

(iii) Kwasababu Yesu baada ya kutoka kuomba, aliona wanafunzi wake wamelala hawaombi, ndipo akamwambia Petro, “Je, Hamkuweza kukesha pamoja nami hata saa moja? (Mathayo 26:40)

(iv)  Yesu aliomba tena mara ya pili, akasema, Baba yangu, ikiwa haiwezekani kikombe hiki kiniepuke, nisipokunywa, mapenzi yako yatimie (Mathayo 26:42)

(v) Aliwakuta wamelala, maana macho yao yamekuwa mazito (Mathayo 26:43)

(vi) Mara ya tatu (Mathayo 26:44)

6.      Pilato aliyekuwa liwali (Mathayo 27:2)

7.      (i) Yuda alijuta akawarudishia wakuu na makuhani na wazee vile vipande thelathini vya fedha. (Mathayo 27:3)

(ii) Alisema, Nalikosa nilipoisaliti damu isiyo na hatia (Mathayo 26:43)

(iii) Alikimbia na kujinyonga. (Mathayo 27:5)

(i) Rangi nyekundu (Mathayo 27:27)

(ii) Mateso aliyopata Bwana Yesu
             (a) Walimuwekea taji la miiba kichwani
             (b) Alipewa mwanzi katika mkono wake wa kuume
             (c) Wakamsalimia kwa kusema “Salamu mfalme wa Wawayahudi”
             (d) Walimtemea mate
             (e) Wakachukua ule mwanzi na kumpigapiga kichwani
             (f) Walinvua vazi lao na kumvika mavazi yake na kumsulubisha.            
             (Mathayo 27:28)

Comments