RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

MCHORO WA OBAMA 'AKISULUBIWA' WAZUA KIZAZAA KWA WAKRISTO


Katika hali inayoonekana kutovumilika, wakristo nchini Marekani wameijia juu picha ya mchoro wa Rais Obama, anayeokana kama akisulubiwa, mfano wa ilivyokuwa kwa Yesu msalabani.
Picha hiyo ambayo imechorwa mnamo miaka 4 iliyopita, na kushindwa kuwekwa hadharani kutokana na hasira zilizoamshwa kwa baadhi ya waumini wa dini ya Kikristo, imerejea tena, na sasa ikiwekwa hadharani kwa ajili ya watu kuiona na kuitathmini jijini Boston kwenye chumba cha maonyesho cha chuo cha jamii cha Bunker Hill hadi 15 december, ijapokuwa baadhi ya watu kulalamika kudhalilishwa kwa dini ya kikristo.
Mchoro huo unamuonesha Rais Obama akiwa anavuta mapazia kufunika nembo ya ikulu ya Marekani, huku akiwa amevishwa taji la miba, jambo lililozua hasira kwa watu.
The Truth © Michael D'Antuono

Licha ya hasira z\a watu kuonekana dhahiri, mchoraji wa picha hiyo, Michael D'Antuono anaonekana kusikitika kwa kuwa mchoro huo umechelewa kufika kwenye hadhira.
"Ninasikitika kwamba mchoro huu uliondolewa kwenye maonyesho mjini New York, natamani usingeondolewa miaka minne iliyopita, nashangaa sana watu wanaokasirika, hawajui kwamba mimi nimetumia haki yangu ya kikatiba kuelezea maoni yangu, hata kama yanawakera wao" Anasema Michael.
Kufuatia kupata tangazo la kuwa picha hiyo itakuwa hadharani, mtangaza nia ya kugombea urais mwaka 2012 kwa kupitia chama cha Republican, Herman Cain, alionekana kuchukizwa na kusema ya kwake.
Hata hivyo kutokana na mfululizo wa mashambulizi kuwa makali, imemlazimu msanii huyo kutoa picha nyingine (What I Meant)kama sehemu ya kutafsiri kile alichomaanisha, na hapa ndipo alipoibua hasira za aina nyingine ya watu, wakimtuhumu kuwa mbaguzi wa rangi kutokana na kuchora watu wengo, akiwemo mtu mmoja mweusi.
What I Meant ©Michael D'Antuono
Mwisho wa yote, msanii huyo aliishia kujitetea kuwa nia yake ni kutaka kumilika uroho na unafiki, na kuwapa changamoto watu kuhusiana na namna wanavyowazua mambo. Tazama baadhi ya kazi zake hapa
CP

thx GK

Comments