RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

NAIBU WAZIRI WA VIJANA, UTAMADUNI NA MICHEZO AKUTANA NA WANAMZIKI WA INJILI NA WACHEZA FILAMU TANZANIA



Kwa mara nyingine tena kimefanyika kikao kikubwa kati ya wadau na viongozi mbalimbali wa muziki na filamu na Mheshimiwa Makala (Naibu waziri wa habari, vijana, utamaduni na michezo)
Kikao hicho kimefanyika katika  ukumbi mdogo uliopo gorofa ya tisa katika ofisi za wizara hiyo. Lengo la kikao hicho ni wasanii kufahamishwa jinsi serikali ilivyojipanga kuwasaidia wasanii wa Tanzania, ili wanufahike na kazi zao na kuwajengea heshima zaidi.
Katika kikao hicho chama cha muziki wa Injili Kimewakilishwa na  Addo November, John Shabani, Bahati Bukuku, Upendo Kilahiro, Cosmas Chidumule, George Mpella na Stella Joel.
  Mwimbaji wa nyimbo za Injili Bahati Bukuku, akizungumza wakati wa Mkutano na Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Amos Makalla, jijini Dar es

Msanii JB akizungumza wakati wa Mkutano huo leo jijini, Dar es Salaam
 Naibu Waziri wa Habari, Vijana Utamaduni na Michezo, Amos Makalla akiwa na baadhi ya wasanii



 Naibu Waziri, Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Amos Makalla akizungumza na wasanii alipokutana nao katika Ukumbi wa Wizara hiyo jijini Dar es Salaam leo

Comments