RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

PICHA ZA MKESHA WA MSIBA WA ASKOFU KULOLA KANISANI TEMEKE

Angalia baadhi ya picha kutoka kanisa la E.A.G.T Temeke jijini Dar es salaam ambako ndiko ulipo msiba wa aliyekuwa askofu mkuu wa kanisa hilo la Evangelistic Assemblies of God, marehemu Dkt. Moses Kulola aliyefariki dunia jana asubuhi jijini Dar es salaam.

Mchungaji Florian Katunzi wa City Centre ambaye anahusika na taratibu za msiba, akizungumza na wenzake msibani hapo.

Watu wakibadilishana mawazo.

Kina mama nao wapo msibani hapo kumsindikiza askofu Kulola.

Waombolezaji wakipata chakula msibani hapo.

Askofu Bruno Mwakibolwa mwenye shati ya kitenge akiwa na mwenzake katika kikao.

Kikao cha baadhi ya watumishi wa E.A.G.T jimbo la Temeke.

Mwimbaji wa nyimbo za injili nchini Flora Mbasha ambaye pia ni mjukuu wa marehemu Kulola akirejea msibani hapo usiku akitokea hospitalini ambako alikuwa amepelekwa baada ya kuzimia msibani hapo.

Emanuel Mbasha kushoto akizungumza na wafiwa wengine msibani hapo.

Mjane wa askofu Kulola akimuuliza mjukuu wake Flora anaendeleaje baada ya mwimbaji huyo kuingia ndani.

Flora akiwa na bibi yake mke wa marehemu askofu Kulola.





Wafiwa wakiwa ndani msibani hapo.

Mwimbaji Rebecca Imagaba akimtukuza Mungu.



New Jerusalem Choir watoto wa Mito ya baraka wakiimba msibani hapo.







Innocent hakuwa nyuma katika kumsifu Mungu.

Mambo ya muziki na vipaza sauti yalikuwa sawa.

Ambilikile akimsifu Mungu mahali hapo, anaushuhuda mzito wa maisha yake na jinsi Mungu alivyomtumia askofu Kulola kumponya.



Uimbaji ulikuwa mwema na mzuri usiku wa kumakia leo.

Comments