RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

WATU ZAIDI YA 20 WARUDISHWA KUTOKA KWENYE MISUKULE HUKO ARUSHA KWENYE MKUTANO WA MCH. GWAJIMA.

Habari inatoka Gospel Media News

Mch. Gwajima akifundisha katika Mkutano

Ni siku nyingine kubwa ambayo Mchungaji Josephat Gwajima ameendelea kutumiwa na Mungu katika Mkutano Mkubwa wa Injili mkoani Arusha. Ikiwa ni siku ya sita leo hii kumetokea mambo ya Ajabu kupita akili za watu kwani watu zaidi ya ishirini ambao walikuwa wamechukuliwa msukule na kupelekwa mikoa mbali mbali kurudishwa.

Akiongozwa na Roho Mtakatifu kuomba kwa kuita watu waliokuwa wamechukuliwa; Mchungaji Gwajima aliomba maombi ya nguvu na kuamuru wote waliochukuliwa warudi. Zifuatazo ni shuhuda mbalimbali za siku ya leo na mambo ambayo Mungu ametenda siku ya leo.

Baadhi ya watu waliorudishwa kutoka kwenye Misukule
Wa kwanza kutoa ushuhuda alisema kuwa yeye anaitwa Neema, alikua amechukuliwa na kupelekwa zanzibar ametoka huko kwa kuruka na alichukuliwa na mke wa shemeji yake.

Mwingine ambaye jina lake halikupatikana kwa haraka alidai kuwa yeye alichukuliwa na kupelekwa Unga Limited.

Mtu wa tatu kutoa ushuhuda; yeye alisema kuwa alikuwa amechukuliwa na bibi yake na kwa jina anaitwa Mary. Kazi yake huko alikuwa analima viazi na walikuwa wanakunywa damu za watu.




Flora na Emmanuel Mbasha wakihudumu katika Mkutano huo
Ushuhuda mwingine uliovuta hisia za wengi ni wa binti wa kiislam aliyeitwa Mwajuma; yeye alisema kuwa alikuwa tabora, ghafla akiwa huko akasikia sauti ikimwita NJOOO akajiona anapaa hadi uwanjani, Arusha. Wakati anasikia sauti hiyo alikuwa katika kazi za kawaida huko za kulima na kazi nyingine aliyokuwa anafanya msukuleni ni kusababisha ajali. Chakula cha huko kilikuwa ni nyama za watu na damu. Mwajuma alisema hataki tena kuwa Muislamu na wachawi wapigwe kwakuwa wanatesa watu wengi maana kuna wengine amewaacha huko wengi.

Ushuhuda mwingine ni wa binti anayeitwa Husna; yeye alikuwa tanga na alichukuliwa msukule na shangazi yake baada ya kulishwa sumu na kufa, ndugu zake waliona amekufa kumbe yeye alikuwepo msukuleni.

Mwingine aliyepata nafasi ya kutoa ushuhuda anaitwa Pendo; yeye alikuwa makaburini alichukuliwa na mama mmoja ambaye hakumkumbuka kwa haraka bali alisema; mama huyo alikuwa mrefu. Mama huyo alimwambia kuwa anampenda na akamchukua akawa anafanya kazi ya kusafisha makaburi ndipo alipopata nafasi ya kumchukua na kumweka msukuleni kwenye makaburi hayohayo aliyokuwa akisafisha.


Baadhi ya Umati wa watu wakiwa Mkutanoni

Mwingine aliyerudishwa alisema kuwa anaitwa Nipha na alichukuliwa akapelekwa Moshi. Akiwa msukuleni akasikia sauti ikimwita NJOO akapaa kutoka moshi; ambapo huko aliwekwa kwa mganga wa kienyeji kwenye kobe ya kuagua.

Msichana mwingine pia alitoa ushuhuda wake kuwa alikuwa Tanga, na jina lake anaitwa Zerina; binti huyo alisema huko Tanga alikuwa anakaa kwenye maji kwenye maji, huko alipelekwa kwa babu mmoja anaitwa hussein alikua hali chakula na alikaa kwa mateso sana.

Mwingine aliyepata nafasi ya kutoa ushuhuda alikuwa anaitwa Rose ambaye yeye alichukuliwa msukule na kupelekwa kibosh. Jina lake ni Rose; alikuwa analishwa nyama za watoto wadogo. Rose alichukuliwa na mke wa mwisho wa baba yake anaitwa Magreth, alisikia sauti kutoka huko akajiona anapaa hadi mkutanoni.

Wa mwisho kushuhudia alisema yeye alikuwa anaitwa Esther na alichukuliwa msukule na kupelekwa Sumbawanga. Yeye alichukuliwa na jirani yake hapo katika mtaa anaoishi.

Comments