RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

PADRI ATAHADHARISHA NDOA ZA JINSIA MOJA, UZAZI WA MPANGO

Imeelezwa kuwa kuna hatari ya familia kwa nchi zinazoendelea ikiwamo Tanzania kufikia ukomo wa ustawi na furaha na pamoja na kujenga taifa lisilo na uhai wa nguvu kazi na lenye maadili kutokana na ndoa za jinsia moja zinazoshika kasi katika mataifa ya Ulaya na Amerika.

Padri wa Kanisa Katoliki nchini amesema kuwapo kwa mazingira hayo matokeo yake ni watu kukoma kuzaa watoto na kukosa familia.

Padri Angelus Shikombe alisema hayo wakati wa ibada maalumu ya siku ya Sherehe ya Familia iliyofanyika katika Kanisa Katoliki la Mtakatifu Bikira Maria la mjini Geita.

“Hali hiyo ikichangiwa na kivuli cha utandawazi, ndoa moja ni suala ambalo hatukubaliani nalo..kwani linachimbia kaburi ustawi wa familia siku zijazo nchi itakosa vijana',” alidai Padri Shikombe.

Padri Shikombe ambaye pia ni Katibu wa Askofu wa Jimbo la Geita mahubiri yake ambayo yalionekana kuwagusa mamia ya waumini, yalisababisha vicheko na wengine kuguna.

Alisema maadili ya Kanisa ni kwamba hakuna ukomo wa kuzaa, ingawa mataifa makubwa yamebuni mpango wa uzazi wa kisasa ambao unaweka ukomo ambao hata hivyo, alisema utasababisha athari kwa mataifa yamayoendelea.

“Ndugu zangu, mataifa makubwa sasa yanatushinikiza kuwepo na ndoa ya jinsia moja na ukomo wa kuzaa mtoto mmoja ni mbinu ya kutuangamiza baada ya mataifa hayo kujikuta hayana vijana wala nguvu kazi ya vijana, yamebakiwa na wazee na sasa yanataka nasi tuwe hivyo,” 'alisema Shikombe.

CHANZO: NIPASHE

Comments