RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

ALIYEKUWA DANCER WA BONY MWAITEGE BWANA CLAUDY P. MWAKALASYA AACHIA ALBAMU YAKE

 Claudy P. Mwakalasya
Baada oya muda mrefu wa kumtumikia Mungu kwa njia ya kucheza, sasa Mungu ameweza kumuinua tena Claudy P. Mwakalasya kwa kumpa karama nyingine ya uimbaji. Kabla ya uimbaji Claudy akiongea na Rumafrica alisema alikuwa na hamu sana ya kuonana na Bony Mwaitege ili aweze kufanya naye kazi ya kumtumikia Mungu.

Siku ya kwanza ya kuonana na Bony Mwaitege anasema ilikuwa ni muujiza kwake kwani hakutegemea kabisa kuonana naye kutokana na Bony kuwa busy sana na huduma. Alipopaya mpenyo tu, cha kwanza alimuomba ampe nguo yake avae ili apate upako kama wa Bony Mwaitege.

Bony alimkaribisha nyumbani kwake na kuanzia hapo Claudy aliweza kufanya kazi ya Bwana na mtumishi wa Mungu Bony Mwaitege. Kuna mengi ametueleza Claudy P Mwakalasya, wewe endelea kutembelea blogu hii...

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgepz1sOueauMm_3Srhmr8j4_j0ZO4ABW5PdikI98w3RibcfWUqpEfRmiWWP_3quCXCMzjfO2q0YmIUbfbC8MjQ78twO5EWKBoFbhVDExw-OqkmDRA07V0fPuH-nHexCOZ9mcEG1zHKMEjC/s640/P1.bmp
Bony Mwaitege


Comments