RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

MUNGU KWANZA RED CARPET KUFANYIKA KESHO NDANI YA URAFIKI SOCIAL HALL . USINIDONDESHE MDAU WA RUMAFRICA KUFIKA MAHALI HAPO

Yamebaki masaa watu wa Mungu kujumuika katika Mungu Kwanza Red Carpet katika ukumbi wa Urafiki Hall kuanzia saa 5:00 asubuhi. Hakutakuwa na kiingilio kabisa. Utakuwa unajiuliza hiki ni kitu gani, lakini siku utakapofika ndio utaamini na kujua kumbe kuna watu wa Mungu ambao  ni wabunifu kwa utukufu wa Mungu.

Umefika sasa wa watu wa Mungu kufanya vitu vipya vyenye utukufu kwa Mungu na kuachana na yale mawazo ya zamani ya kilokokole kama vile ya kusema ukipendeza ni dhambi na ukila chakula kizuri ni dhmabi. Huu ni wakati ambao watu wa Mungu wa kuonyesha kuwa Mungu naye anahitaji vitu vizuri na sio vibaya.

Leah Amos

Watu wa Mungu tumekuwa wavivu sana katika maswala yahusuyo Mungu, hatuna suport kabisa na tunabaki kulalamika kuwa wokovu ni kama kifungo kwani hakuna raha kama za watu wa kidunia. Haya mazingiara tunayatengeneza wenyewe na sio mtu mwingine. Tunatakiwa kuwaunga mkono hasa watu ambao Mungu amewapa ubunifu wa kufanya wonders ili wazidi kubuni vikubwa sana, tuache kukatisha tamaa.

Sasa katika Mungu Kwanza Red Carpet ninakuomba usinidondoshe, natamani kukona eneo hilo ukiwa umependeza huku ukizungukwa na upako wa Kristo. Kumbuka kutotenda dhambi kila kuitwapo leo.



Joshua Silomba

Nisamehe kama nimekuchosha ila nimeamua kufunguka ili nitoe kilichomo ndani yangu, inaumiza sana kuona watu wanataka kufanya kazi ya Mungu thalafu kunakuwa hakuna suport...Mbaya sana.


Daniel Waipungu


Katika issue hii iliyombele yetu kuna kundi la Mungu Kwanza kesho litajitambulisha rasmi kwa wadau wa muziki wa injili Tanzania katika ukumbi wa Urafiki Social Hall uliopo Legho-Sinza.


Emmanuel Peter


Kutakuwa na Waimbaji wengi kuhudhuria tamasha hili ikiwa m ni pamoja na waimbaji chipukizi kutoka lebal{kampuni} ya pamoja kwa umoja waimbaji hao ni:  Emmanuel Peter, Joshua Steven , Joshua Silomba, Leah Amos, Daniel Mwaipungu
na wengine wengi.


Jitahidi usikose

Wenu katika  Bwana
Rulea Sanga

Comments