RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

FAIDA ZA KUHUDHURIA MIKUTANO

Utapata Faida Gani Ukihuzuria Mikutano Yetu?

Watu wengi wameacha kwenda katika makanisa yao, kwa sababu wanapokwenda huko hawapate majibu ya maulizo ya lazima wanayojiuliza maishani na hawapate faraja. Basi, sababu gani wewe unapaswa kuhuzuria mikutano ya Mashahidi wa Yehova? Kuhuzuria mikutano hiyo kutakuletea faida gani?
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjvmKf1dd3ab42CsaMZJ2aTMNIt7Dv9Sp2XGV8haT1YOu7YaUrc0RSMwPE_zxNAC8wRMxruhkIrC7sSpLKbFeLuwVC367aMZ0ejH3LBYm6QHC791gdrggHXe_qy_tuwZc0_MMDP-rzT/s1600/08.jpg

Utapata furaha kwa sababu utakuwa kati ya watu wanaokupenda na kukuhangaikia.
Wakati wa mitume, Wakristo walikuwa katika tengenezo moja lililokuwa na makutaniko, na walifanya mikutano ili kumuabudu Yehova, kujifunza Maandiko, na kutiana moyo. (Waebrania 10:24, 25) Kwa sababu walionyeshana upendo kwenye mikutano, walijisikia kuwa kati ya marafiki wa kweli, ni kusema, ndugu na dada zao Wakristo. (2 Wathesalonike 1:3; 3 Yohana 14) Sisi pia tunafuata mufano huo wa Wakristo wa kwanza, na kwa hiyo, tunakuwa wenye furaha kama wao.
http://lh6.ggpht.com/--_toJnCsnRk/T7umK6HrxAI/AAAAAAAACXs/l9zdpvus4V0/DSCN0501_thumb%25255B2%25255D.jpg?imgmax=800

Utajifunza namna ya kutumia kanuni za Biblia katika maisha yako.
Kama ilivyokuwa wakati wa zamani, wanaume, wanawake, na watoto wanakusanyika wote pamoja. Walimu wenye kustahili wanatumia Biblia ili kutusaidia kujua namna ya kutumia kanuni za Biblia katika maisha yetu. (Kumbukumbu la Torati 31:12; Nehemia 8:8) Kuna sehemu za mikutano hiyo zinazoomba wahuzuriaji pia waseme; ni kusema, watoe pia maelezo ao majibu na wakati wa kuimba nyimbo kila mutu anaweza kuimba pamoja na wengine. Kwa kufanya hivyo, tunaeleza tumaini letu mbele ya wengine.—Waebrania 10:23.

Utapata faida nyingine; imani yako itatiwa nguvu.

Mutume Paulo aliandikia kutaniko moja hivi: ‘Ninatamani kuwaona ninyi, kwamba kuwe na ubadilishanaji wa kitia-moyo kati yenu, kila mumoja kupitia imani ya mwengine, yenu na yangu pia.’ (Waroma 1:11, 12) Kukusanyika na ndugu na dada zetu kwa ukawaida kunatia imani yetu nguvu na hilo linatufanya tuwe na nguvu ya kuheshimu kanuni za Biblia katika maisha yetu.

Basi, sababu gani usipange kuhuzuria mikutano yetu ili ujionee wewe mwenyewe mambo hayo? Utakaribishwa kwa furaha. Kuingia ni bure na hautaombwa kutoa sadaka.

Comments