Bloggers wengi wenye malengo ya muda mrefu na blogs zao pamoja
bloggers wapya bado wanachanganyikiwa sana kuhusu platform ipi ni muhimu
kuitumia kwenye blogging. Tanzania kwa sasa kuna mushrooming ya blogs,
yaani kuwepo kwa blogs nyingi SANA! Ni jambo zuri kwamba watu wanajikita
zaidi kwenye tech na ni “mzuka” tu wa kuwa na blog ndio unaowashika
watu kwa sababu mwisho wa siku blog hizo hufa. Kinachonifurahisha zaidi
ni jinsi ambavyo asilimia 70 ya heading ya blogs zetu utakuta “WELCOME
TO MY WORLD”! Simlengi mtu yoyote but if the shoe fits feel free to
wear it. Kama hiyo na wewe ndio heading yako, be creative, jitofautishe
na wengine!
Yote ya yote, kuna platform nyingi za blogging lakini mbili kubwa ni blogger.com na wordpress.org
Blogger.com ina faida nyingi, na baadhi ni hizi:
1. Ni rahisi kutumia kwa bloggers wapya
Kufanya setup ni rahisi. Unafuata hatua tu na kuingiza details chache, basi!
2. No need to install anything.
Hauna haja ya kufanya installation yoyote! Kila kitu muhimu kipo by default.
3. Ni bure kutumia
As a beginner, hii ni platform nzuri ya kuanzia ka sababu utajifunza
basics nyingi ambazo zitakuwezesha kuzoea blogging na ni bure.
4. Kuweka posts ni rahisi
Kuandika post ni rahisi. Ni sawa na kuchapa kwenye Ms Word tu.
5. Rahisi kubadilisha Theme
Kama hauna uhakika na jinsi blog yako inavyoonekana, unaweza
ukabadilisha ndani ya sekunde moja tu! Hii inaafanya bloggers wapya
wajue jinsi unavyoweza kutumia designs tofauti tofauti kwenye blogging.
6. Dashboard moja
Blog zako zote za blogspot utazipata katika sehemu moja tu tofauti na
platform nyingine kama wordpress ambapo inabidi kila moja uifungue
kivyake.
HASARA ZA KUTUMIA Blogger.com:
1. Limited flexibility
Ka sababu kuna designs na themes chache, most blogs look and feel the
same. Blogs nyingi zinafanana na zina feel the same. Hii inamaanisha
hauwezi kujitofautisha na bloggers wengine kwa sababu mnafanana kwa
ukaribu sana.
2. Domain Name ndefu sana.
Since blog yako iko hosted na blogger.com, domain name yako itakuwa na brand yao kama:
www.jinalablogyako.blogspot.com badala ya kuwa na domain kama
www.jinalablogyako.com
Visitors na wateja wako watajua kuwa umetengeneza kwa kutumia
blogspot. Sio mbaya ingawa binafsi naona haipendezi watu kujua unatumia
ninii. hata for security reasons, inakuwa rahisi kwa hacker
kukushambulia akishajua unatumia nini. Kuhusu domain, unaweza ukanunua
ya kwako ingawa ndio tayari utakuwa umeingia gharama nyingine.
3. Mmiliki HALISI wa blog yako anabaki kuwa Blogger.com!
Kama ulikuwa hujui, ni kwamba wewe hauimiliki blog yako iwapo ni ya
blogspot. inamaanisha iwapo siku Blogger ikifungwa au ikiuzwa,
inamiliki blog yako na kila kitu kwenye blog yako. Unless ulifanya
backup sehemu, basi ndio utakuwa umepoteza kila kitu. Kama Blogger
(yaani Blogger.com) wakiamua kwamba hawaipendi blog yako, wanaizima muda
wowote.
Kama una maswali au kuna msaada uanhitaji, comment hapa chini.Kama una mpango wa kutengeneza hela online, unaweza kuanzia blogger ili ukue jinsi blogs zinavyofanya kazi. Baadae, unaweza kuhamia platform nyingine wanazotumia bloggers wazoefu.
Kama una maswali au kuna msaada uanhitaji, comment hapa chini.Kama una mpango wa kutengeneza hela online, unaweza kuanzia blogger ili ukue jinsi blogs zinavyofanya kazi. Baadae, unaweza kuhamia platform nyingine wanazotumia bloggers wazoefu.
Comments