RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

ISIS WAENDELEA KUFANYA MAUAJI YA KUTISHA HUKO SYRIA NA IRAQ

WAPIGANAJI wa ISIS wamefanya mauaji ya kutisha kwa mateka wawili wa kiume waliotuhumiwa kuwaua kwa kuwapiga virungu wanawake watatu huko nchini Iraq.

ISIS waliwapiga watuhumiwa hao kwa matofali ya zege kichwani hadi kufa ikiwa ni adhabu kwa kitendo chao cha kuiba na kuwaua wanawake watatu. Tukio hilo limefanyika katika Mkoa wa Nineveh huko kaskazini mwa Iraq.

Katika tukio lingine lililowekwa katika mitandao ya kijamii wiki hii linaonyesha picha za wanaume wawili wengine wakichinjwa na kundi hilo la ISIS katika Kijiji cha Jarnyah, Magharibi mwa Raqqa nchini Syria.

Wanaume hao wanadaiwa kuuawa baada ya kukamatwa wakijihusisha na vitendo vya kishirikina.

Wanaume hao waliokuwa wamefungwa vitambaa usoni wanaonekana wakiwa wameweka vichwa vyao juu ya magogo huku mapanga yakiwa kwenye shingo zao na wananchi wakishuhudia tukio hilo.

Wiki iliyopita, picha za wapiganaji hao wa ISIS wakiwapiga mawe hadi kufa mashoga wawili huko Syria nazo zilionekana kwenye mitandao ya kijamii.

Kabla ya kuwaua mashoga hao, ISIS waliachia picha zilizokuwa zikiwaonyesha mashoga hao wakiwa wamekumbatiana na kuwaambia kuwa wamewasamehe dhambi zao kabla ya kuwapiga kwa mawe hadi kufa.
Mpiganaji wa ISIS akinyanyua tofali la zege kumpiga mmoja wa wanaume waliokamatwa kwa kuua wanawake.


Adhabu ya kuwapiga mawe wanaume waliokamatwa kwa mauaji ya wanawake watatu ikiendelea huko Iraq.

Mmoja wa watuhumiwa wa uchawi akiwa tayari kuchinjwa na Kundi la ISIS huko Raqqa, Syria.


Mtuhumiwa mwingine wa uchawi naye akiwa tayari kuchinjwa na ISIS.


Kabla ya kuuawa watuhumiwa hao walisomewa mashtaka yao na mmoja wa wapiganaji wa ISIS.

Picha ya mashoga wawili waliowekwa mitandaoni na Kundi la ISIS kabla ya kuwapia mawe hadi kufa.

Mashoga hao wakipigwa mawe hadi kufa na wapiganaji wa ISIS huko Syria.

Comments