MCHAKALIKAJI KATIKA KUINUA NA KUJENGA MWILI WA KRISTO, MESS CHENGULA AMEACHIA WIMBO MPYA FT UPENDO NKONE
Tanzania tumebahatika sana kuwapata vijana wanaohangaika kwaajili ya kazi ya Mungu. Mess Jacob Chengula ni mkinga kutoka Makete ambaye kwa sasa makazi yake yako Dar es Salaama Tanzania na mfanyabiashara maarufu sana Kariakoo kwa upande wa Spare Parts. Hivi karibuni ameamua kuachia wimbo wake mpya ambao amemshirikisha mwaimbaji mashuhuri sana Tanzania, Upendo Nkone. Wimbo huu unaenda kwa jina la MOYO HAUNA WOGA TENA. Kaaeni mkao wa kula wadau wake
Comments