Mistari
hii 10 ya Biblia inatukumbusha kwamba hatuko peke yetu. Daima Mungu yu
pamoja nasi. Pokea nguvu kupitia neno la Mungu na umimine moyo wako
kwake yeye anaye yajua mahitaji yako yote na hujibu pale unapolitia jina
lake.
Yohana 14:18
Sitawaacha ninyi yatima; naja kwenu.
Yoshua 1:5
Hapatakuwa
mtu ye yote atakayeweza kusimama mbele yako siku zote za maisha yako;
kama nilivyokuwa pamoja na Musa, ndivyo nitakavyokuwa pamoja na wewe;
sitakupungukia wala sitakuacha.
Isaya 41:10
Usiogope,
kwa maana mimi ni pamoja nawe; usifadhaike, kwa maana mimi ni Mungu
wako; nitakutia nguvu, naam, nitakusaidia, naam, nitakushika kwa mkono
wa kuume wa haki yangu.
Zaburi 27:10
Baba yangu na mama yangu wameniacha, Bali Bwana atanikaribisha kwake.
Kumbukumbu La Torati 31:8
Naye Bwana, yeye ndiye atakayekutangulia, atakuwa pamoja nawe, hatakupungukia wala kukuacha; usiogope wala usifadhaike.
Zaburi 62:8
Enyi watu, mtumainini sikuzote, Ifunueni mioyo yenu mbele zake; Mungu ndiye kimbilio letu.
1 Yohana 4:13
Katika hili tunafahamu ya kuwa tunakaa ndani yake, naye ndani yetu, kwa kuwa ametushirikisha Roho wake.
Zaburi 94:17
Kama Bwana asingalikuwa msaada wangu, Nafsi yangu kwa upesi ingalikaa penye kimya.
Zaburi 145:18
Bwana yu karibu na wote wamwitao, Wote wamwitao kwa uaminifu.
Yeremia 29:11
Maana
nayajua mawazo ninayowawazia ninyi, asema Bwana, ni mawazo ya amani
wala si ya mabaya, kuwapa ninyi tumaini siku zenu za mwisho.
Comments