RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

MATUKIO YA CHAMA CHA MUZIKI WA INJILI KILIVYOFANYA KAZI YA MUNGU JIJINI MWANZA

Waimbaji wa nyimbo za Injili waliomo ndani ya Chama Cha Muziki wa Injili Tanzania (CHAMUITA) wamefanyika baraka kubwa kwa wakazi wa jiji la Mwanza kwa huduma yao ya uimbaji na maombezi. Chama hiki kiliamua kuongozana na Mch. Dkt. Rejoice Ndalima kuelekea Mwanza kwa lengo la kuliombea Taifa la Tanzania amani na utulivu wakiungana na wakazi wa jiji la Mwanza. Kama tunavyotambua kuwa nchi yetu ya Tanzania ipo katika kipindi cha Uchaguzi Mkuu wa Tanzania, kwahiyo kama watumishi wa Mungu tunalazimika kukaa miguu pa Bwana na kumuomba Mungu wetu azidi kuipa amani nchi yetu ili yasitokee machafuko ya kivita na kuruga amani yetu.

Waimbaji hawa waliweza kupata muda wa kuwaombea wakazi wa Mwanza na kukemea mapepo yaliyokuwa yakiwasumbua kwa muda mrefu. Hakika Mungu amekuwa mwema kwao, na nguvu za Mungu zilijidhihirisha kwa wananchi wa Mwanza.

Chama hiki kipo kwaajili ya kutetea haki za wanamukizi wa Injili Tanzania na pia kusaidiana wakati wa shida na raha. Na pia chama hiki kimesajiliwa na ni chama cha Kitaifa. Waimbaji hupata muda wa kufanya maombi kila mwisho wa mwezi na pia kufanya sifa kwaajili ya utukufu wa Mungu.

Wakazi wa Mwanza walionyesha upendo wa ajabu sana kwa wageni wao kwa kuwaandalia chakula na malazi bure kabisa. Kongamano hili lilileta msisimko mkubwa sana kwa wakazi wa Mwanza na hakika waliweza kujifunza kitu kwa waimbaji hawa kutoka Dar es Salaam na mkoa mbalimbali.

KIPINDI CHA WAANDISHI WA HABARI WA MKOA WA MWANZA WAKIFANYA MAHOJIANO NA VIONGOZI WA CHAMUITA KUJUA MENGI KUHUSU CHAMA HICHO.

 Kulia ni Ulimbaga Mwakatobe na kushoto ni Katibu Mwenezi Taifa Stella Joel
 Mmoja wa viongozi wa CHAMUITA Magreth Sembuche akiwa na Ulimbaga Mwakatobe
 Baadhi ya viongozi na wenyeji wa mkoa wa Mwanza wakihojiwa
Katubu Mwenezi wa CHAMUITA, Stella Joel


KIPINDI CHA MAOMBEZI NA UPONYAJI KIKIENDELEA
 Madam Ruti (kulia) na Magreth Sembuche - wote ni waimbaji na viongozi wa CHAMUITA kutoka Dar es Salaam
 Madam Ruti akiombea wakazi wa Mwanza

Madam Ruti

KIPINDI CHA KUSIFU NA KUABUD

Ulimbaga Mwakatobe

Stela Joel kulia akiimba

Madam Ruti

Magreth Sembuche

KIPINDI CHA KUSIKILIZA NENO LA MUNGU KUTOKA KWA WATUMISHI WA MUNGU
 Askofu Dkt. Rojice Ndalima kutoka Dar es Salaam (kushoto) akisikiliza Neno la Mungu akifutia Madam Ruti na Magreth Sembuche
BAADA YA KAZI NZITO YA BWANA ULIFIKA WAKATI WA KUPATA CHAKULA
 Magreth Sembuche
 Ulimbaga Mwakatobe
 Stella Joel
Magreth Sembuche

KIPINDI CHA KURUDI DAR ES SALAAM KILIWADIA

Ulimbaga Mwakatobe akiwa kwenye ndege kurudi Dar akitokea Mwanza

ANGALIA MATUKIO MENGINE YALITOKEA JIJINI MWANZA NA WANACHAMUITA KWA KUBONYZA HAPA

Comments