RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

KONGAMAONO KUBWA LA SHILOH KUTIKISA TANZANIA KUANZIA TAREHE 06.11.2015 KATIKA KANISA LA MLIMA WA MOTO ASSEMBLIES OF GOD MIKOCHENI "B" DAR ES SALAAM

Kwa watu waliohudhuria Shiloh mwaka jana ukiwaambia kuhusu Shiloh watakusimulia jinsi Mungu wetu anavyojitokeza kwa watu wake kupitia siku hizi 7 za Shiloh. Shiloh ni kongamano ambalo hufanyika kwa mwaka mara moja katika kanisa la Mlima wa Moto Assemblies of God Mikocheni "B" kwa lengo la kuwakusanya watu kutoka dini tofauti na makabila tofauti  kukaa pamoja na kumtafakari huyu Mungu wetu, na pia huwa kunakuwa na mambo mengi sana yanayoendelea mahali hapo. Shiloh ya Mwaka itafanyika kwa kipindi cha wiki moja tu ambapo watu wataweza kujumuika pamoja na kumtukuza Mungu. Katika Shiloh ya mwaka huu  kutakuwepo  na waimbaji mbalimbali na watumishi wa Mungu mbalimbali kama vile  Askofu Dastan Maboya na watumishi wengine wengi, pia kutakuwepo na waimbaji kama Goodluck, Bahati Bukuku, Furaha Isaya, Happy Choir, Joy Bringers, Mass Choir ya Mlima wa Moto, Gideon Mutalemwa na wengine wengi sana.
Unakaribisha sana ili uweze kupokea baraka za Mungu wetu kupitia Shiloh


DVD na AUDIO CD za Mahubiri ya Shilloh zitapatikana


RED CARPET ITAKUWEPO SIKU HIYO YA SHILOH

WAHUDUMU WATAVALIA BADGES ZAO

BANNER ZITATAPAKA KILA KONA YA JIJI


STICKER ZA KUPANDIKA KWENYE MAGARI ZINAPATIKANA SASA
 ZAWADI MBALIMBALI ZITAKUWEPO KWA KAMA UTAJIBU MASWALI VIZURI KUPITIA PRAISE POWER RADIO
WHEEL COVERS KWAAJILI YA KUTANGAZA SHILOH NA KAZI YA MUNGU

Comments