RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

IBADA YA JUMAPILI MLIMA WA MOTO SI YA KUPUUZIA, NJOO UONE NEEMA ZA BWANA MAISHA MWAKO

Unaweza ukawa umehudhuria ibada nyingi katika makanisa mbalimbali na hukuweza kupata jibu lako kutokana na sababu zisizoambilika, ila leo hii tunakushauri kufika katika kanisa la Mlima wa Moto siku ya kesho ili uweze kuona mkono wa Bwana ukigusa maisha yako na utaona mpenyo wa mabadiliko katika kazi zako na familia yako. Unachotakiwa kufanya ni kuja ukiwa na IMANI ya kuwa, Bwana anakwenda kutenda jambo fulani katika maisha yako.

Umehangaika sana kutafuta faraja, lakini leo nasema umechagua njia sahihi ya kuja kwa Bwana kupitia kanisa la Mlima wa Moto. Bishop Dr. Gertrude Rwakatare amekuandalia Neno la Mungu ambalo ukitoka nalo unakwenda kubadilika na kuwa mtu mwenye mvuto kwa jamii yako, kila mtu atatamani kukaa na wewe na kupata ushauri kutoka kwako. Mungu akusaidie Jumapili tuonane Mlima wa Moto Mikocheni "B" jijini Dar es Salaam, Tanzania

Comments