RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

MCH. NOAH LUKUMAY WA KANISA LA MLIMA WA MOTO AFUNDISHA JUU WA "MTU WA NNE" SIKU YA JUMAPILI 10.04.2016- KIPENGELE CHA KWANZA: ACHA KUHANGAIKA NA MAKANISA

Mch. Noah Lukumay katika ibada ya Jumapili 10.04.2016 aliweza kuhubiri Neno la Mungu na kuwaonya watu kutulia katika kanisa moja na sio kutangatanga kwani wanaweza kupata madhara, na hivi ndivyo alivyohubiri, “ Sasa cha ajabu ni kule mitaani na kwenye makanisa mengine ambayo yatakunywesha vitu ambavyo havifai, yaani ukafunguliwe mahali ambapo mtu anakwambia lala nikulalie, nipite juu ya mgongo wako.
Bishop Dr. Gertrude Rwakatare akifuatilia somo

 Unajuwa duniani kuna vituko yaani kuna mwingine anataka akufanyie deliverance alale juu ya mwili wako, mwingine atembee juu ya mwili wako, sasa utaona ninayetaka kukufanyia delivareance nina kilo 90 halafu wewe una kilo 50 halafu mimi nipite juu yako ninatembea kitakachotokea nitakuvunja vunja tu. Sasa unapoanza kuhangaika na makanisa inakuja kuwa tatizo. 
Mzee wa kanisa akiwa akitafakari

Sasa utakapokuja hapa tutashindwa kukukomboa kwa sababu umekuja na matatizo mengine kutoka kwenye makanisa mengine, kwa hiyo ni lazima utambue kwamba kuna watumishi wa MUNGU waliopakwa mafuta ili waweze kukutoa katika roho zilizokushikilia, ili wakutoe katika vifungo vilivyonishikilia. 
Unajua mafuta yanatofautiana;- Yaani mimi na Bishop Dr. Gertrude Rwakatare kuna mahali Bishop anacheza peke yake mimi siwezi kwa hio inabidi yeye awe juu yangu halafu yale mafuta mimi niyachote niyaachilie kwa watu, kwa sababu yeye ni kisima na mimi ni bomba, amina. Kwahiyo nakuomba sana utulie katika kanisa moja ili uweze kubarikiwa na kufunguliwa, acha kuhangaika na makanisa.






Comments