RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

EPHRAIM SEKELETI AIONGELEA ALBUM YAKE MPYA



Muimbaji nguli wa Muziki wa injili kutoka nchini Zambia Ephraim Sekeleti ameiambia Hosanna Kwanza kuwa mwaka huu wa 2016 anatarajia kuiweka sokoni album yake mpya iitwayo MUNGU USIYELALA.Akiongea kutoka nchini Zambia Ephraim amesema mpaka sasa kupitia kampuni yake ya Ephraim Media Company amekwisha kamilisha Video ya wimbo huo uliobeba jina la album ilihali all audio songs tayari zishakamilika.

Ephraim aliyejulikana sana nchini kwa album yake ya kwanza ya Kiswahili yenye nyimbo ya UNIONGOZE pamoja na BARAKA ZAKO na nyingine nyingi,amesema album yake hii mpya itakuwa na Ubora zaidi kuliko ile ya kwanza.Kwa sasa Ephraim yuko busy akitafuta watu sahihi wa kuwekeza katika muziki wake.


Sekeleti na Mkewe