RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

UNAPOANGUSHWA IPO SIKU UTASIMAMA TENA, BISHOP DR. GERTUDE RWAKTARE

Bishop Dr. Getrude Rwakatare siku ya Jumapili 15.05.2016 katika ibada ya KUFUNGULIWA iliyofanyika Mlima wa Moto Mikocheni “B” alikuwa na haya ya kusema, “Tusome AYUBU 22:29, Hapo watakapokuangusha utasema kuna kuinuka tena? Naye mnyenyekevu MUNGU atamwokoa. 

Mch. RAHA kutoka Marekani

Watu wabaya mdio wanakuangusha kirejareja lakini kuna Neno la faraja utaenda nalo, sasa kila mtu akikabidhi njia zake kwa BWANA kabla ya kufanya lolote hakika huyu ni mcha MUNGU. Jamani dunia ni mbaya lakini jipeni moyo kwa maana Yesu ameushinda ulimwengu, watu watakuangusha lakini usiogope kwa sababu kuanguka siyo mwisho wa safari, inafaa uinuke tena n uendelee mbele, ukiendelea mbele ni lazima utashinda. Watu wa MUNGU ni kama wapiganaji wa masumbwi wanapigana yaani kama watu wanapigana ngumi unaweza ukamuona damu inamtoka puani unaweza ukasema ndio imekwisha lakini atalala chini watahesabu 1, 2, 3, utaona miguu inasimama, na watu wanaanza kushangaa na kusema, huyu mtu tulizani amekufa kumbe ni mzima mara ameinuka na damu zake, na hata sisi watu wa MUNGU sisi tu sawa sawa na wapigana masumbwi, hata kama tulianguka lakini tutainuka tena. Hata kama ulishindwa utashinda tu, hata kama wanakucheka wewe leo ni maskini kesho utakuwa tajiri tu, hata kama leo umekuwa ni mgonjwa kesho utakuwa ni mzima. Usikate tama, msikate tamaa wala usimkatie tamaa mtu maadamu ana MUNGU wake MUNGU atakuja, MUNGU ataingilia kati, Bwana asifiwe sana. Usikose Jumapili saa 3 asubuhi kanisani Mlima wa Moto Mikocheni ”B”


 Mch. Raha kutoka Marekani (kulia)

 Wachungaji wa Mlima wa Moto Mikokocheni "B" - Mch Otieno (kushoto) na Mch. Francis Machichi (kushoto)

 Mch. Elizabeth (wa pili kutokam kushoto)