RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

BISHOP DR. GERTRUDE RWAKATARE: NIONGEE NA WEWE UNAYEUMWA SASA

“Leo nataka kuongea na ugonjwa unao kusumbua, wengine wanasumbuliwa na BP, Pressure, kwa Yesu yote ni sifuri. Leo naenda kuongea na UKIMWI, haijarishi una UKIMWI kwa Yesu unasaluti amri. Mwingine leo ameambia ana Kansa, au anauvimbe kwenye tumbo la uzazi au damu zinamtoka ovyo, leo nina habari njema kwako, Neno la Mungu linasema “Wala hakuna mwenyeji wa Mlima wa Moto atakaye sema mimi mgongwa, atakayesema mimi naumwa wote wakaao ndani ya Mlima wa Moto watasamehewa dhambi zao watakuwa wazima na afya”, pokea afya njema kwa jina la Yesu, pokea uponyaji kwa jina la Yesu, pokea mume kwa jina la Yesu. Magonjwa ni tatizo ya ulimwengu mpaka wakaweka shirika lile la Health Organization kushugulikia utafiti wa magonjwa ya aina mbalimbali. Pengine unajisikia kunoga kujikuna na ukijikuna unasikia maji yametoka na ukipeleka kwenye jicho pamevimba ukipeleka hapa pametoboka yaani mwili umejaa madonda mwili mzima, magonjwa kama hayo na mengine mengi kama hayo yamelishika Taifa ili afe mwanadamu. Huenda umetumikia magonjwa mbalimbali kadha wa kadha wanatafuta dawa za kisukari , dawa za UKIMWI, wanatafuta dawa za Pressure lakini hawapati wamebaki kunanyamazisha tu maumivu lakini leo hii na habari njema kwako leo Mwisho kwako, Daktari wa Madaktari yupo anayeweza kuponya UKIMWI, Utasa, Kisukari, Presha leo undoka na uponyaji wako, hautotoka kama ulivyoingia kwa jina la Yesu utatoka mzima nimeyafunga kwa jina la Yesu Neno la Mungu linasema, “Hakuna mwenyeji atakayesema mimi mgonjwa”, wengine wanasema kiuno changu, mguu wangu, macho yangu huna macho magonjwa Yesu alikuumba ukiwa mzima, wewe huna kiuno kinachokuuma ni shetani amekubambikizia magonjwa leo tunamchanachana, tunamkanyaga kata magonjwa kwa jina la Yesu toka magonjwa katika maisha yangu huna nafasi kwangu, huna mamlaka katika jina la Yesu”. Hivi ndivyo alivyosema Bishop Dr. Gertrude Rwakatare Jumapili 18.09.2016. Mlima wa Moto Mikocheni “B”