nilikuwa na jambo ambalo nimependa niwaambie
Waimbaji hasa waliotangulia kusikika ama kujulikana na jamii napenda wawe na ushirikiano mzuri na waimbaji hawa wanaochipukia
Maana huwa wanalalamika Sana kuwa hawapati ushilikiano mzuri hasa pale anapomfata mwimbaji aliye juu kumuomba ushauri
Juu ya uimbaji wake au unakuta Kama Mwimbaj wa kike anaechipukia akimfata Mwimbaj wa kiume aliye juu kimziki kuna Maneno anaambiwa yule binti hadi anavunjika moyo kabisa jamani waimbaji tuenende Kama atakavyo
Mungu wetu sote tuitangaze injili ya Bwana wetu Yesu kristo nimependa sasa hivi kuna vipaji vingi vinachipukia na wanafanya vizuri katika soko na katika Media nimependa uwimbaji wao kama huyu Dada Oliver Wema ukimsikiliza uwimbaji Wake Kama Rose Mhando sio Kama anamuiga bali ndiyo sauti yake na yeye aliyopewa na
Mungu napia unakuta niupenzi unajua ukimpenda mtu basi utataka ufanye kama yule mtu unayempenda ndiyo maana huwezi kuwatofautisha
mwimbaji mwingine nimeanza kusikia nyimbo zake hivi karibun maradion anaitwa Debora Lusinde huyu Dada nae uwimbaji wake ukiusikia ni Kama Mather mwaipaja
Ukiiyona video ndiyo utatambua kuwa siyo Mather kwaiyo napenda kwasababu wote wanamtukuza Mungu mmoja kwa njia ya uimbaji naombeni tuwe na ushirikiano watu wa Mungu.