RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

MCH. NOAH LUKUMAY: MAOMBI “SPECIAL” KWA WAGONJWA

“Sema damu ya Yesu shuka ndani yangu, ondoa sumu yoyote iliyokaa kwenye damu yangu, ikiwa ni sumu ya madawa ambazo nimekula, damu ya Yesu ondoa hiyo sumu.”

Kuna watu ambao hawawezi kula chakula bila dawa kila masaa yanavyokwenda, anakumbuka dawa zilipo. Maisha yake ni ya madawa. Utasikia akisema, “Leo dawa zangu nimesahau”, badae anaanza kusikia nusu kifo kinamsogelea. “Sema kwa jina la Yesu, kila mifuko ya madawa ambazo shetani ametufungia, leo nakataa kwa jina la Yesu kila kifurushi cha madawa kwenye mwili wangu shetani naziondoa kwa jina la Yesu”.

Sema, “Eee Bwana Yesu, wewe ni kiboko, kila tatizo siku ya leo linakwenda kuisha, ninaenda kuinywa damu ya Yesu ambayo inatakasa maisha yangu kwa jina la Yesu”. Sema, “Damu ya Yesu twketeza virusi vya magonjwa yote vinavyoshambulia mwili wangu kwa jina la Yesu”. Nani anayeuwa chembechembe zako haI ambazo zinashambulia magonjwa kabla la kupata dawa? Kuna mapepo, kuna uchawi, ambayo yanashambulia chembechembe zako. Nasema, sasa hivi lazima uziamuru chembechembe zako kama zimelegea zipate nguvu kwa kunywa damu ya Yesu kwa imani, na hii damu itafufua kilichokufa na kikikutana na damu ya Yesu kitakuwa hai.

Sema, “Kwa jina la Yesu ninapokea damu ya Yesu kwa imani ninapoenda kuinywa, na kama kuna chembechembe hai zimekufa ndani yangu, kwa kupitia damu ya Yesu zikaamke tena kwa jina la Yesu. Kila chembechembe hai ambazo zimechoka kupitia damu ya Yesu leo zikaamke. Amen. haya ni maombi ya Mch. Kiongozi Noal Lukumay siku ya Jumapili 18.09.2016