RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

VIDEO: MH.PAUL MAKONDA AMEAHIDI KUJENGA STUDIO YA GOSPEL. AONGEZA MILIONI 3 GSS




Mkuu Wa Mkoa Wa Dar Mhe. Paul Makonda Aongeza Zawadi Za Washiriki Wa Gospel Star Search.   Top Ten Wa Gospel Star Search Walitembelea Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa kama Njia ya Kujitambulisha Kwake. Vijana hao wanaotoka Katika Jiji la Makonda Walijitambulisha na Kisha Kuimba Mbele ya Mkuu wa Mkoa.

Mkuu Wa Mkoa ameahidi kutoa Shilingi Milioni Moja Moja kwa Washiriki namba 1 hadi 3 na kisha kuanzia saa 4 hadi 10 kila mmoja atapata laki mbili mbili. Mbali na Hilo Mkuu wa Mkoa ameahidi Kujenga Kituo Maalum Kwa ajili ya Kukuza Waimbaji wa GSS.

Gospel Star Search inafikia fainali siku ya Jumapili ya Tarehe 18 September, 2016 katika Ukumbi wa Mirado kuanzia saa 9 alasiri. Tiketi ni sh. 10,000 kwa viti vya kawaida na Sh. 20,000 kwa viti Maalum. Kwa Mawasiliano zaidi piga namba 0713494110