Jumapili ya jana,Oktoba 9 katika kanisa la Victory Christian Center Tabarnacle mwimbaji mahiri wa nyimbo za Injili Tanzania Angel Benard aliweka alama nyingine katika jiji la Dar kupitia tamasha lake la IT’S ON ambapo ni mwendelezo wa ziara zake za nchi nzima za kuwakusanya wana wa Mungu na kuabudu pamoja.
Katika tamasha hilo lililokuwa na mguso wa kipekee halikudhirihisha tu kipawa alichokirimiwa Angel Benard lakini kibali na mafuta ambayo Mungu ameweka ndani yake.Watu walijtokeza kwa wingi kumsifu na kumwabudu Mungu pamoja na Angel ambaye alisindikizwa na waimbaji wengi kama The rivers of Joy,Elly Joh,Paul Clement,Bomby Johnson,Robert,The Doxaz,Goodluck Gozbert na wengineo.
Tamasha hilo lililoanza mishale ya saa tisa lilifunguliwa na sifa na kuabudu kutoka kwa The Rivers of Joy kutoka VCCT na baadaye kuafatiwa na Gospel rapper Elly Joh kutoka Borne Kingz
Elly Joh akihudumu
Baadhi ya watu waliohudhuria tamasha hilo
Ikafika zamu ya The Doxaz kumwadhimisha Bwana..