RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

07.12.2016: BISHOP DUNSTAN MABOYA NA BISHOP DR. GERTRUDE RWAKATARE WAKIWAOMBEA WATU WENYE MAGONJWA SUGU KATIKA SHILOH TANZANIA 2016 NDANI YA KANISA LA MLIMA WA MOTO MIKOCHENI "B" SIKU YA JUMATANO


Bishop Dunstan Maboya siku ya Jumatano 07.12.2016 katika kusanyiko la SHILOH TANZANIA 2016 ndani ya nyumba ya BWANA Mlima wa Moto Mikocheni "B" kwaakishirikina na mwenyeji wa kusanyiko hilo Bishop Dr. Gertrude Rwakatare aliweza kuwaombea watu wenye magonjwa sugu kama kansa na uvimbe. Kuna baadhi ya watu walipokea uponyaji hapo kwa hapo baada ya kuwaombea na kuwaomba wamguse Bishop Dr. Gertrude Rwakatare ambaye naye aliweza kutamka maneno ya uponyaji kwa watu hawa. Tuna kila sababu ya kumshukuru Mungu kwa uponyaji huo, kwani walio wengi walitoka wakiwa na furaha na kicheko na wengine wakitoa machozi ya furaha kwa matendo makuu waliyotendewa na Mungu.

Shiloh hii ya 2016 imekuwa baraka kwa walio wengi. Mungu amekuwa akiwashangaza watu kwa miujiza na wengine kupata amani ya mioyo yao, na wengine wakipata faraja kutokana na kukata tamaa. Mungu ni mwaminifu sana kwa wale wanaoamini na kutii sheria zake. Yawezekana wewe una mali nyingi lakini bado unateseka na magonjwa, madeni makubwa, kutukanwa kwasababu ni mgumba, kutopata watoto, kukosa amani ya moyo wako, unaishi maisha ya wasiwasi na shida mbalimbali, umejaribu kuhangaika huku na kule bila ya majibu. Lakini leo sauti ya Mungu inakuita njoo na ungana na wenzako katika SHILOH hii kwani utapata wepesi wa maisha yako. Mungu atakupa kile unachohitaji kwa wakati autakao yeye, usikate tamaa, amua sasa kuja kwa Yesu.

Ratiba ya SHILOH: Kuanzia saa 4 asubuhi hadi saa 8 mchana ni maombezi na saa 9 mchana hadi 12 jioni ni Ibada kuu ya SHILOH.

Rev. Ndeda kutoka Afrika Kusini ameshawasili na tayari ameanza kuhudumia watu na kuachilia upako wa mafanikio kat0ika maisha ya watu. Jitahidi uwezavyo kuungana na wenzako katika SHILOH hii ya Kihistoria.












 Mzee mwenye tatizo la kusikia akiombewa
 Mzee mwenye ugonjwa wa Kisukari, hawezi kusikia vizuri na mguu kumsumbua aliombewa