07.12.2016: BISHOP DUNSTAN MABOYA NA BISHOP DR. GERTRUDE RWAKATARE WAKIWAOMBEA WATU WENYE MAGONJWA SUGU KATIKA SHILOH TANZANIA 2016 NDANI YA KANISA LA MLIMA WA MOTO MIKOCHENI "B" SIKU YA JUMATANO
Shiloh hii ya 2016 imekuwa baraka kwa walio wengi. Mungu amekuwa akiwashangaza watu kwa miujiza na wengine kupata amani ya mioyo yao, na wengine wakipata faraja kutokana na kukata tamaa. Mungu ni mwaminifu sana kwa wale wanaoamini na kutii sheria zake. Yawezekana wewe una mali nyingi lakini bado unateseka na magonjwa, madeni makubwa, kutukanwa kwasababu ni mgumba, kutopata watoto, kukosa amani ya moyo wako, unaishi maisha ya wasiwasi na shida mbalimbali, umejaribu kuhangaika huku na kule bila ya majibu. Lakini leo sauti ya Mungu inakuita njoo na ungana na wenzako katika SHILOH hii kwani utapata wepesi wa maisha yako. Mungu atakupa kile unachohitaji kwa wakati autakao yeye, usikate tamaa, amua sasa kuja kwa Yesu.
Ratiba ya SHILOH: Kuanzia saa 4 asubuhi hadi saa 8 mchana ni maombezi na saa 9 mchana hadi 12 jioni ni Ibada kuu ya SHILOH.
Rev. Ndeda kutoka Afrika Kusini ameshawasili na tayari ameanza kuhudumia watu na kuachilia upako wa mafanikio kat0ika maisha ya watu. Jitahidi uwezavyo kuungana na wenzako katika SHILOH hii ya Kihistoria.
Mzee mwenye tatizo la kusikia akiombewa
Mzee mwenye ugonjwa wa Kisukari, hawezi kusikia vizuri na mguu kumsumbua aliombewa